As-Samiry – Mtengeneza Ndama wa Sanamu

As-Samiry – Mtengeneza Ndama wa Sanamu.

Haiwezekani Mtume wa Allah Harun kuwa ndie aliyetengeneza ndama na kulingania ushirikina: Mitume wote walikuwa ni walinganizi wa Tawhid. Atakayenukuu yasiyokuwa hayo amepotoka, mfano wa hayo yaliyokuja: “Harun akawaambia: Zivunjeni pete za dhahabu zilizo katika masikio ya wake zenu, na wana wenu, na binti zenu, mkaniletee. Watu wote wakazivunja pete za dhahabu zilizo katika masikio yao, wakamletea Haruni. Akaipokea mikononi mwao akaitengeneza kwa patasi, akaifanya iwe sanamu ya ndama kwa kuiyeyusha; na wakasema, Hiyo ndiyo miungu yako, Ee Israeli, iliyo kutoka katika nchi ya Misri.” (Kutoka: 32/2-4). Agano la kale.


Tags: