Starehe ya Kiroho.

Starehe ya Kiroho.

“Kinachonishughulisha mimi sasa hivi ni ninachokipata katika neema za dini. Kama vile ambavyo ninajali neema tunayopata kutokana na umeme, chakula bora na maji safi. Haya yote hutusaidia kuishi maisha mazuri yenye neema. Ama dini hunipa mengi zaidi ya haya. Hunipa raha starehe ya kiroho, au hunipa (kama aliyozungumza William James) msukumo wa nguvu wenye kuunganisha maisha. Maisha yenye nafasi, yenye furaha maridhawa, kwa hakika inanipa imani, matarajio na ujasiri na huniondolea khofu, sononeko na wasiwasi. Vile vile hunielekeza kwenye malengo katika maisha na hukunjua mbele yangu upeo wa furaha na kunisaidia katika kujenga chemchem ya maji na rutuba katikati ya jangwa la maisha yetu.”


Tags: