Kuwasaidia wengine kukabiliana na matatizo

Kuwasaidia wengine kukabiliana na matatizo

“Kuna utafiti unaothibitisha kuwa mtu kuwasaidia wengine ni tiba ya babaiko la nafsi, wataalamu katika saikolojia wanathibitisha kwamba kuwasaidia wengine hupunguza wasiwasi na msongo wa mawazo ambapo kushughulika kwa hima katika kuwasaidia wengine huhamasisha kutoa Homoni aina ya hormone endorphins nayo ni homoni yenye kumsaidia mtu kuhisi raha ya kinafsi na hisia za juu za furaha, Alan Leeks Mkuu wa zamani wa chuo cha “Kukuza Afya” (institute for health promotion) huko Marekani anathibitisha kwamba kuwasaidia wengine husaidia katika kupunguza msongo wa mawazo ambapo mtu kuwasaidia wengine hupunguza mawazo yake yeye mwenyewe binafsi na matatizo yanayomkabili mwenyewe: Na mwisho hupata mwenyewe hisia za raha na utulivu wa nafsi.”


Tags: