YERUSALEM NCHI ZA DINI NA VITA MBALI MBALI

YERUSALEM NCHI ZA DINI NA VITA MBALI MBALI

YERUSALEM NCHI ZA DINI NA VITA MBALI MBALI

(1)

Pamoja na kuwa muda wangu wa kukaa Israeli ni mdogo sana, lakini nitajaribu kutembelea sehemu za Wakristo na alama zao mbali mbali za kumbu kumbu pamoja na kukutana na Wakristo.

Joji alimaliza matayarisho ya safari yake, alijitahidi kumaliza mapema sana, kwa lengo apate muda wa kutosha usiku kwa ajili ya watoto wake na mke wake. Tokea aliporudi kutoka India kazi zilimnyima nafasi ya kukaa na wanawe, kadhalika na vikao virefu vya Kakhi katika kupitia mikataba, akizidisha na kupunguza katika maelezo yake. Hili ni mbali na muda mwingi anaoutumia katika kusoma kuhusu Uyahudi kabla ya safari yake akitamani kutumia ziara yake kwenda nchi ya vita mbali mbali kutafuta majibu ya maswali yake makubwa, na isiishie katika kazi zake tu.
Katarina mpenzi wangu. Je unahitaji chochote kutoka Tel Aviv?
Nakutaka utembelee Kanisa la Kiama, na Kanisa la Bikira Maria na usali ndani yake.
Nimesoma kuhusu Kanisa la Kiama, hili ni kanisa lililojengwa na mfalme mkuu Helen mama wa Mfalme Constantine mwaka 335 A.D. Kanisa lilikamilika kujengwa sehemu ya juu sehemu ambayo iligunduliwa ile mbao ambayo inasemekana kuwa ndio ambayo Bwana Masiya Yesu alisulubiwa. Kanisa lilijengwa kwa muda wa miaka 270, kisha Wafursi waliliunguza walipoiteka Yerusalem, kisha mtawa Modest aliyekuwa rais wa makazi ya watawa akalijenga tena wakati ule katika mwaka 617 A.D. Kanisa hilo lilikarabatiwa mara nyingi, haswa wakati wa Constantine mwaka 1048 A.D. pindi watu wa msalaba walipoteka Yerusalemu mwaka 1099 ambapo walikusanya sehemu mbali mbali za kuabudia katika Kanisa moja ambayo ndio hii iliyosimama leo hii. Pamoja na hayo yote lakini sio tukufu kwetu sisi Waprotestant, ila mimi nitalitembelea na kuswali kwa ajili yako, lakini nitajitahidi kuswali katika Kanisa la bikira Maria vile vile, je unataka kitu kingine?

Asante, inaelekea umesoma mengi kuhusu Yerusalem?

Sio sana naendelea kusoma.

Yerusalem ni sehemu muhimu sana kwa Wakristo na sio Wayahudi; ndani yake pana msalaba wa Yesu, na kuna makanisa mengi ya Kihistoria.

Ahah.. ni kiasi gani nilikuwa natamani kutembelea alama hizi za kumbu kumbu mwenyewe kisha nisali kwa ajili ya Bwana.

Kama ni hivyo kwa nini usije na mimi?

Kwa sasa siwezi, nina shughuli nyingi kazini, kanisani, huenda huko mbeleni baada ya kutuondoshea dhulma tuliyonayo.

Dhulma?!

Mayahudi katika kudhihirisha wanachodai kuwa ni urithi wao wa kitamaduni huko Yerusalem wamedhalilisha Makanisa na Wakristo huko Yerusalem.

Historia ya Yerusalem ni historia yenye kusisimua na migongano yote ya dini za mbinguni, kwa mnasaba katika yanayosemwa kuhusu Yerusalem ni kuwa ilishaangamizwa mara mbili, na kuzungukwa kwa kutekwa mara 23, na kushambuliwa mara 52, kisha wakatekwa na kushambuliwa tena hadi kupoteza ardhi yao tena mara 44. Bado dini mbali mbali za mbinguni zinatarajia vita vikubwa, kwa kweli ni ardhi ya vita, lakini nashangazwa na maneno yako….Uingereza ndio iliyowapa Mayahudi! Kama ni hivyo basi dhulma iko wapi?

Kwa masikitiko ndio, ila ni kuwa kinachokusudiwa –au kinachoitwa kuwa ni –Ahadi ya Balfour ilikuwa na sababu za kisiasa na migongano mikubwa.

Ilikuwaje na ni zipi sababu hizo?

Miongoni mwa sababu zake ni: Uingereza kuingia katika vita vya kwanza vya dunia (19141918); ambapo Uingreza ilikuwa na haja ya msaada wa Mayahudi (kisiasa na kisayansi/kielimu) wakati wa vita vya kwanza vya dunia, kisha wakati huo huo harakati za Wazayuni zilikuwa zinatafuta atakayesaidia mradi wake wa kusimamisha nchi ya Taifa la Wayahudi katika ardhi ya Wapalestina.

Ni mabadilishano ya kimaslahi tu?!

Hapana, kulikuwa na sababu zingine huko Ulaya: Hamu ya watu wa Ulaya ilikuwa ni kuwaondosha Mayahudi Ulaya; kwani kundi kubwa la Mayahudi halikuweza kuchangamana (na watu wengine) katika sehemu walizokuwa wakiishi, na walikuwa wakiishi kama vile kiwiliwili kilichojitenga na dola, na sababu nyingine ilikuwa na lengo la kupanda nguvu nyingine iliyokuwa tofauti huko Palestina ambalo ni daraja linalounganisha Misri na Afrika na baina ya Waarabu na Waislamu huko Asia, na sababu nyingine ni kusawazisha nguvu; nafasi na utawala wa Wayahudi katika baadhi ya nafasi muhimu katika Dola ya Ukhalifa ya Otoman ambayo ilikuwa inahatarisha nchi za Ulaya, na hivyo basi Uingereza ilitaka kuirithi dola hii.

Unaibebesha Uingereza makosa yote!

Hapana kabisa, mimi nabebesha makosa siasa yoyote ambayo haifikirii dini, Je, haikuwa ni kipaumbele kuiteka Yerusalem na kuifanya makao makuu ya Ukristo?

Hivyo kinachotakiwa ni kukalia kwa mabavu katika njia nyingine chini ya Wakristo badala ya Mayahudi!! Ama mimi natofautiana nawe katika rai na naamini kuwa sehemu katika ile ahadi ya Balfour ni ya kidini.

(2)

Ni ipi sababu ya kidini kwa mtazamo wako?

Tafsiri potofu ya mafundisho ya Kikristo ndio ambayo imeifanya harakati za Uzayuni kuenea sana ndani ya kanisa la Kristo na wanasingizia na kuhalalisha matendo yao ya kibaguzi na kijambazi kwa jina la dini.

Samahani hili halipo katika Ukatoliki.

Swadakta liko kwetu – Protestant – sana tena sana, kuna makundi mengi kwetu yanayoamini kuwa kusimama kwa taifa la Israel mwaka 1948 lilikuwa ni jambo lisilozuilika; kwani linatimiza utabiri wa kitabu kitakatifu cha Agano lote la Kale na Jipya, na ni utangulizi wa ujio wa Masiya kwa mara ya pili ardhini kama vile mfalme aliyeshinda. Wazayuni Wakristo wanaamini kuwa ni wajibu wao kuwalinda Mayahudi kwa ujumla na haswa dola yao ya Kiebrania, kisha akatabasamu –na kusema:Ukweli ni kuwa wewe unaukosoa Uprotestant na sio Uingereza, kwa ujumla Israel ni kitu kilicho kweli hivi sasa, na tunaishi na taifa hilo.

Lakini makanisa yetu na sehemu zetu tukufu na maaskofu wetu wasiteswe.

Dhulma ni mbaya sana kwa hali zote, iwe ilikuwa ni kwa Mayahudi au Mkristo, na hii sio mara ya kwanza ambapo Wakristo wanateswa na Mayahudi, ama sivyo?!

Kweli kabisa, kuanzia Yesu ambaye alijitoa mhanga kwa ajili ya wanadamu, ambae aliuawa na Mayahudi, kisha wafuasi wake kuteswa, hadi ndugu zetu wakateswa huko Yerusalem.

Ha ha ha, inaelekea nimeingia katika vita vya dini na mauaji yake kabla hata ya kufika Yerusalem, haya na tulale kabla ya muda kututupa, itabidi niende uwanja wa ndege usiku wa manane.

Joji aliwasili Tel Aviv asubuhi ya alhamisi saa mbili unusu asubuhi na alikuwepo kumpokea, aliona machoni mwake mng’ao unaodhihirisha kuwa ni mtu mjanja mjanja na mwenye uwezo mkubwa wa akili.

Hallo – Karibu katika nchi takatifu Yerusalem.

Asante –ni kiasi gani mimi ni mwenye furaha kwa kufika kwangu katika mji huu mtakatifu.

Kakhi amenijulisha kuwa safari yako itakuwa fupi siku nne tu.

Ndio, sipendi safari za mfululizo, kabla ya kuja kwangu huku nilikuwa India, lakini Kakhi akanisisitiza kwa kunitukuza kwa ziara yangu katika mji mtakatifu.

Nimetayarisha kila kitu, mkataba utasainiwa baada ya siku mbili; hivyo usijali sana, kuwepo kwako tu ni kuhakikisha kuwa mikataba imepitia njia zote za kawaida.

Hii ni nzuri.

Je, utaenda hotelini au kwenye shirika?

Hotelini, ili niweke mkoba wangu, kisha tuelekee kwenye shirika moja kwa moja.

Vizuri, kesho kutwa ni jumamosi na Levi hafanyi kazi jumamosi, huenda ukahitaji kufanya nae kikao leo au kesho, Levi ni mwanamke mwenye dini sana na mtaalamu mzuri wa teknolojia na anachokijali yeye zaidi ni kuwa programu ya ulinzi iwe na nguvu zaidi kuliko uwezo wa magaidi kuiingilia na kuivamia.

Programu ya ulinzi ambayo tumewapeni ni nzuri sana na yenye nguvu, hivyo msihofie hilo.

Kama ni hivyo mthibitishie hilo Levi, na kujali kwako kulinda amani ya Israeli, kwani hili ndilo analolijali zaidi, bali unaweza kushangazwa na mazungumzo nae ambayo yanaweza kukupeleka mbali kwenye mazungumzo ya kiitikadi, kifalsafa na sio kwenye fani ya teknolojia pekee.

Kiitikadi na kifalsafa?!

Ndio, na hii ndio sehemu ya tabia yake mbaya, kwa ujumla kama kuna tabu sana ya kutangamana nae nijulishe, kisha akatabasamu na kusema: Pamoja na inadi yake harudishi matakwa yangu.

Vizuri.

Walifika hotelini, Joji akaweka begi lake, kisha akateremka mara moja kwa na akaelekea kwenye shirika…..Jengo la shirika lenyewe halikuwa kubwa lenye kuvutia, bali lilikuwa la wastani lakini lenye wafanyakazi lukuki, ama ulinzi ndani ya jengo la shirika ulikuwa mkali pamoja na mtaa mzima.
Walikwenda katika ofisi ya , ambaye baada tu ya kufika aliwasiliana na Levi na kumtaka afike.

Matatizo yatakuja sasa hivi.

Matatizo! Kwa nini?

Kasumba yake ya dini humfanya asifahamu maisha kwa njia sahihi, na ni mpenzi sana wa mijadala wala haoni tabu nayo, ingawaje mwishowe hulainika kwa kutumia nguvu.

Baada ya dakika chache akatokezea msichana mzuri sana akiwa amevaa nguo za heshima lakini hazikuweza kuficha uzuri wake, akamtambulisha kwa Joji:

Levi ni mkuu wa kitengo cha teknolojia katika shirika letu… kisha akamuashiria Joji; na huyu ni Joji ndie mhusika wa kitengo cha Programming katika shirika la Advance Electronic huko Uingereza.

Karibu sana, asante kwa kufika kwako, nahitaji maelezo mengi ya kitaalamu kutoka kwako.

Sawa nitafurahi kuyajibu.

Mnaweza kufanya mkutano wenu katika chumba cha mikutano mkipenda.

Vizuri, mr. Joji karibu.

Joji na Levi walikwenda katika chumba cha mkutano, kilikuwa ni chumba kidogo lakini kilichopangwa vizuri na cha kifahari.

Karibu.

Asante sana, inaelekea bado haujatulizwa na Programu ya Ulinzi ambayo shirika letu limewapeni?

Hapana, hili silo kusudio, lakini nilitaka kuwa na tumaini tu. Kwani usalama wetu kama Mayahudi na ulinzi wetu ni jambo muhimu sana na linalonishughulisha sana.

Programu hii ni katika programu yenye nguvu sana ya ulinzi, lakini hisia yangu ni kuwa nyie mna woga unaowafanya mshadidie sana suala la ulinzi.

Unakusudia nini?

Ulinzi niliouona kwenye mtaa mzima na kwenye jengo lenu hili sijawahi kuuona katika maisha yangu hapo kabla.

Sisi ni watu tulioteswa sana katika historia yote, na nadhani jambo langu la msingi ni kuona kuwa kuna ulinzi wa kutosha kwa watu wangu kadiri iwezekanavyo.

Vizuri, kama ni hivyo jukumu langu litakuwa ni kuwasaidia katika suala hili la teknolojia ya ulinzi.

Kutusaidia! Kwa nini utusaidie?

Sifahamu! niwasaidie kwa programu ya pekee ya ulinzi ambayo tutaingia katika mkataba ambao utasainiwa.

Samahani nilichozoea ni kuwa watu wote wapo dhidi yetu sisi Mayahudi.

Mimi ni Mwingereza Mkristo tena Mprotestant, kwani hukumbuki kuwa aliyewapa nchi hii ni Balfour, Mwingereza Mkristo tena ni Mprotestant?

Hii ni nchi yetu na ardhi yetu, na hakuna mtu aliyetupatia na ni wajibu wetu kujilinda wenyewe.

Inaelekea unapenda sana mjadala, je unataka nikuambie ukweli?

Ninapenda sana mjadala na ukweli naupenda na ninautaka.

Kama unapenda ukweli kama usemavyo, wewe unatoka wapi? Inaelekea wewe ni Mzungu?!

Mimi ni Mwisraeli.

Je baba yako na mama yako wamezaliwa Israeli?

Wazazi wangu ni Waustria na walikuja hapa mwaka 1970, na mimi nikazaliwa hapa Israeli, kwa hivyo mimi ni Mwisraeli pamoja na kuwa nina uraia wa Austria.

Hivyo basi wewe ni Mwaustria unailinda Israeli na mimi Mwingereza nakupatia Programu ya Ulinzi.

Lakini mimi ni Myahudi na wewe ni Protestanti!

Je baba yako ni Myahudi?

Hapana, alikuwa Mkristo asiyeamini Mungu lakini Uyahudi unakuja kwa njia ya mama na sio wa baba.

Ukweli ni kuwa nimekuja Yerusalem kwa mambo mawili. Kwanza Kusaini mkataba, na Pili: Nataka kuujua Uyahudi, kwani huenda nikawa Myahudi, Je, tunaweza kuzungumzia zaidi na kwa kina kuhusu dini?

Kwa furaha kabisa, isipokuwa haiwezekani ukawa Myahudi kama mama yako sio Myahudi.

Kwa vipi?

Sisi ni taifa lililochaguliwa, tumechaguliwa na Mungu katika damu yetu na itikadi.

Kwa hivyo basi nyinyi hamlinganii dini yenu (hamuitangazi ili watu waingie)?

Kamwe, ila tunawalingania wasiokuwa sisi ili watuhudumie sisi taifa lililochaguliwa.

Yaani wawe wanawatumikia nyie tu!!

Hapana utumishi bila ya malipo.

Malipo ya kusaini mkataba wa ulinzi, mnatulipa malipo stahiki tuliyokubaliana, huu sio utumishi! Huku ni kuuza na kununua.

Na kama sio mkuu wenu wa shirika Myahudi basi shirika lenu lisingechaguliwa kutupatia ulinzi huo.

Lakini Kakhi ni Msekula!

Wakati huo mfanyakazi akagonga mlango, na Levi akamuuliza Joji angependa apewe nini.…

maji na kahawa….unaonaje tukianza maudhui tokea mwanzo wake?

Karibu, inaelekea unajali sana kujua dini mama, Uyahudi ambayo ni dini mama ya dini zote za mbinguni.

Una maana dini mama wa dini za mbinguni ni Uyahudi na Musa anaaminiwa na Mayahudi, Wakristo na Waislamu.

Ndio, waliofuatia baada ya hapo watu walitofautiana kuhusu wao, Mayahudi hawamuamini Yesu na Wakristo hawamuamini Muhammad.

Tunaweza kusema kuwa Waislamu huamini wote, na Mayahudi hawaamini zaidi ya mitume yao… achana na hilo, nataka kujua kutoka kwako Uyahudi kwa undani zaidi, Je unaweza kunisaidia?

Unaelekea wewe kuwa ni mwanazuoni wa dini nyingi na sio mtaalamu wa Programming! Karibu.

Joji alikusudia ndani ya nafsi yake kupambana na Levi na kumvuta kidogo kidogo; ili aweze kujua kwa undani kuhusu Uyahudi kwani hataki apate kutoka kwake maelezo ya juu juu tu bali ukweli.

Ni ipi itikadi ya Mayahudi kuhusu mungu? Wanamueleza vipi, au wana mjuaje?

Sifahamu unachotaka kukijua? Lakini mungu ndie muumba na mtoa riziki.

Nimesoma mambo mengi kuhusu sifa ya mungu kwenu ambazo sijazifahamu bali zimeniletea matatizo; katika nilichosoma katika Agano la Kale: “Na maneno ya Mungu kwa Samueli yalikuwa: Nimejuta kwa nini nimemfanya Saoli Mfalme.” Na katika agano la kale kitabu cha ‘Kutoka’ nimesoma: “Akasikika minong’ono yao Mungu akakumbuka agano lake pamoja na Adamu, Isaka na Yakobo.” Kadhalika nimesoma katika kitabu cha Hesabu kauli yake Mungu. “Ondoka sasa ukawapige na uwaharamishie mali zao, na usiwasamehe, bali muue kila mwanamme na mwanamke na mtoto na anayenyonya na ng’ombe na mbuzi na ngamia na punda.” Na mifano mingi kama hiyo, mara nyingi najiuliza: Je, Mungu anajuta, anasahau na kukumbuka na anaamrisha kuuwa na kutosamehe? Ni mungu gani huyu?

Inaelekea unasoma sana, lakini tatizo lako unachagua la kusoma, ulilolisema ni sahihi na mengineyo mengi lakini jambo hilo sio haswa kwa Uyahudi tu? Hata nyie mna zaidi ya mara tatu ya hayo yetu.

Ha ha ha, swadakta tunayo mifano mingi ya namna hiyo ndio maana nafikiria kuwa Myahudi, unaonaje tumalizie mazungumzo yetu kuhusu itikadi za kiyahudi baadae, nilitaka tumalizie suala la mikataba leo hii na kesho; kwani kesho kutwa ni Jumamosi na nyie hamfanyi kazi.

Kweli kabisa: Jumamosi ni siku ya mapumziko na ibada, bali katika wasia kumi yamekuja mafundisho ya kudumu na kulihifadhi jambo hili nayo ni siku ambayo Mungu alimaliza kuumba mbingu na ardhi na akapumzika Jumamosi.

Alipumzika?!

Ndio alipumzika, inaelekea una hisia kali katika baadhi ya matamshi kuhusu Mungu, hili ni tatizo lako.

Huenda ikawa hivyo, la msingi tumalize mjadala wetu kuhusu mkataba kwa muda wa siku mbili, nami nimeanza kuhisi uchovu leo hii kwani nimetokea uwanja wa ndege hadi kwenye shirika lenu.

Unaweza kwenda kupumzika sasa hivi, tumalize mazungumzo yetu jioni ukipenda.

Je haitokuwa dhiki kama tutamalizia mazungumzo yetu hotelini baada ya saa kumi unusu?

Bila ya shaka….nitakuja hotelini kwako saa kumi unusu.

Kama ni hivyo tule pamoja, huenda ukawa na utulivu zaidi, na ukapunguza ukali wako katika kuamiliana nami.

Sifahamu unakusudia nini?! Wewe umenishambulia sana leo, samahani kama nimekukosea.

Mimi ndie wa kuomba msamaha kama nimekushambulia, kwa mtu mwenye uzuri kama wewe haifai kushambuliwa na kukerwa.

Huu ni wema wako, lakini mashambulio yako ya hapo kabla nimeyapenda kuliko kujitenga kwako hivi sasa –kisha akatabasamu na kusema: Mimi naishi maisha yangu kwa ajili ya Mungu tu.

Kabla ya kuondoka nataka kumsalimia .

Sawa, karibu.

Waliondoka pamoja kwenda ofisi ya , akawauliza swali kuhusu mkutano wao….

Mjadala ulikuwa mzuri na wenye faida.

Nawaombeni ruhusa ili nirejee kwenye kazi zangu?

Karibu ewe Levi, lakini Joji ni mgeni wetu ni lazima tumkirimu.

Vizuri, kwa heri.

Tumekubaliana niende hotelini kupumzika kidogo, na Levi atakuja hotelini tumalizie mjadala.....nimefahamu kwa nini sisi tuna haja ya siku mbili kwa uchache ili kusaini mkataba, yeye anapenda mjadala sana.

Fikra ya kumaliza mjadala hotelini ni nzuri, kwani inaondosha baadhi ya urasimu.

Ndio, lakini Levi anaelekea mgumu sana!

Pamoja na ugumu wake lakini ni mwema na tabia yake ni nzuri, na nitamjulisha aache inadi yake na ukali wake wa kutoshawishika kabla ya kuja kwake kwako leo hii.

Hamna neno, naomba ruhusa, nahisi nimechoka kidogo.

Karibu, dereva atakupeleka hotelini.

Karibu, dereva atakupeleka hotelini.

(3)

Joji alifika hotelini saa saba na nusu mchana alipanda chumbani mwake na
kujinyoosha kitandani hakukawia akawa amelala, hakuamka hadi ilipotimu saa kumi na robo… aliosha uso wake haraka haraka na kubadilisha nguo zake.
Mara simu ikalia chumbani…alikuwa ni mhudumu kwenye mapokezi ambae alimjulisha kuwa kuna mwanamke anayemsubiri jina lake Levi….Joji aliteremka haraka akamuona Levi na nywele zake nyekundu, na nguo zake
zisizo za kazini inayoonesha namna anavyojiheshimu lakini nguo zile ni
za mkesha.Joji alimpa mkono; akatabasamu tabasamu ang’avu iliyoonesha uzuri
wake na kumvutia sana…

Unaonekana mzuri zaidi kuliko ulivyokuwa asubuhi!

Asante kwa rai yako.

Tafadhali twende tukale, natumalizie mazungumzo yetu wakati tutakapokuwa tunakula.

Walichagua meza ya peke yake iliyojitenga pale hotelini, wakakaa hali ya kuelekeana… Joji alimuita mhudumu na wakaagiza walichotaka…

Unaonaje wakati wa kula tusizungumze chochote kuhusu kazi?

Kama utakavyo…

Wewe ni mzuri sana, je umeolewa?

Hapana, bado, nilidhani mnatofuatiana na Kakhi.

Ki vipi?

Wewe unajali sana mambo ya dini na torati na injili, wakati ambapo Kakhi hajali isipokuwa mali na wanawake..

Ni kweli lakini ni kitu gani ambacho tunafanana?

Nilidhani hupendi mali sana, wala uzuri haukushughulishi….

Ni nani ambae hajali wala hapendi mali na uzuri? Lakini sijafahamu una kusudia nini!

amezungumza nami baada ya kutoka kwako kuhusu makusudio ya mkutano kufanyika hotelini.

Unakusudia nini?

Wewe ni kama Kakhi unataka starehe…starehe tu.

Nibainishie zaidi!

Usijifanye mjinga, mimi nipo tayari.

Joji alijifanya hajui kinachoendelea, na hafahamu mafumbo yake…

Nami nipo tayari vile vile kumalizia mjadala wetu, lakini baada ya kumaliza chakula changu.

Vizuri, lakini je ungependa mjadala motomoto?

Kama upendavyo.

Sipendi kumkatalia jambo , vile vile kama upendavyo.

Ni nini uhusiano wa katika mjadala wetu?!

Niache niseme… Nyie wanaume hamjali chochote isipokuwa ni ngono tu.

Inaelekea kuwa mimi nazungumzia jambo fulani na wewe unazungumzia jambo lingine kabisa!

Joji alianza kufahamu vizuri zaidi, na akaunganisha mazungumzo ya Levi na maneno ya Kakhi na , na pindi walipotoka hotelini kula chakula Joji alielekea kwenye bustani iliyopo nje na kumwambia Levi:

Napendekeza tukae katika bustani ya hoteli kama utaliona hilo linafaa?

Bustanini!! Kama utakavyo!!!!

Inaelekea ni sehemu nzuri na inafaa kupeana ukweli.

Ndio ni sehemu tulivu, lakini ipo wazi mbele za watu, unataka nini?

Ninataka tujadiliane.

Je unanifanyia mzaha? Nimekuambia kuwa amenizungumzia na mimi tayari nimeshajitayarisha.

Nami nipo tayari tuanze mjadala, kisha akaendelea; kuna sintofahamu kutoka kwa : Mimi sio Kakhi.

Nilichofahamu kutoka kwa kuwa nyie ni wamoja; na ndio maana nimejitayarisha kama uonavyo.

Je hukuniambia kuwa hupendi kusifiwa kwa mapenzi na kuwa maisha yako ni kwa ajili ya Mungu tu!

Mimi…mimi nimekubali kumhudumia Mungu.

Kumhudumia Mungu! Vipi?

Jambo muhimu zaidi katika ibada ya Mungu ni: Kutumikia Dola ya Israeli na kuwatumikia watu wake wateule wa Mungu.

Na wewe kwa masikitiko ni mwanamke rahisi sana? Je huna uwezo kuwa huru katika nafsi yako kwa uchache!

Kwa sababu umeanza kunishambulia, nitazungumza kwa ukweli: mwanamke katika Uyahudi ana sehemu yake maalum, wala muamala wake si kama wa wanaume, na sipendi kuzungumzia hilo, je tunaweza kubadilisha maudhui?

Sijafahamu, nami sipendi kuzungumza hilo wakati wewe hupendi hilo, lakini hukuniambia hapo kabla kuwa wewe unapenda mjadala!

Mimi napenda sana mjadala, lakini nahofia kufahamika vibaya… nataraji unifahamu kwa njia sahihi.

Tafadhali, haya niambie.

Jinsia na mwanamke katika Uyahudi inahitaji maelezo, kwa mfano kiasili kwetu sisi mahusiano ya kawaida yaliyo sahihi kuhusu jinsia (ngono) yanatakiwa yawe kwa lengo la kuzaa tu, nayo ni kati ya mke na mume. Hata hivyo kwa masikitiko –mwanamke amedhalilishwa na hufanywa kama mtoto mdogo au mwenda wazimu au mnyama, naye hutumika kwa starehe tu, imekuja kwenye Talmud: “Kwa hakika mwanamke ni mkoba uliojaa mavi”….kisha akageuka kwa hasira, na kusema: Je hili ndilo utakalo?! Je unataka ukidhi haja yako kwenye mkoba huu?!

Samahani kwa kukukera, naliona hili jambo ni la dhulma sana na ubaguzi, na tukamilishe mazungumzo yetu kwa utulivu na kitu gani kinachokulazimisha uwe hivyo?

! na kumtii!

Sifahamu! Nini uhusiano kilichopita na utiifu wako usio wa mipaka kwa .

ni mume wa mama yangu.

Baba yako!

Hapana, hapana, baba yangu alikufa kwenye bomu la gaidi Muislamu… hivyo baba yangu mdogo akamrithi mama yangu, kwani imekuja kwenye Torati: “Imefaradhishwa kwa mwanamke mjane kwa ndugu wa mume wake.”

Amerithiwa na ndugu ya baba yako? Kwani hiyo ni bidhaa ili irithiwe?!

Ndio, kwa masikitiko hulazimishwa kuolewa na ndugu wa mume wake.

Samahani sio kwamba sikuamini, lakini unachozungumza sikiamini! Na nadhani unaikosoa sana torati pamoja na kudai kuwa wewe ni Myahudi na mwenye dini!

Aah huenda nikawa nimezidisha kubwabwaja! na sipendi mazungumzo haya, lakini wewe ndie unayetaka! Kisha akapumua na kuangalia chini: Pamoja na kujali kwangu kutokusema chochote hadi hivi sasa.

Je kuna zaidi ya yale uliyoyasema?!

Macho mazuri ya Levi yalijaa machozi, akahema na kusema:

Kwa kuwa wewe ndie uliyetaka, kwa bahati mbaya ndio! Ushahidi wa wanawake mia moja ni sawa na ushahidi wa mwanamme mmoja! Mwanamke ni kiumbe shetani, na yupo chini kuliko mwanamme!...Imekuja kwenye torati: “Ni wajibu kwa mwanamme asipite baina ya wanawake wawili au mbwa wawili au nguruwe wawili, kama vile ambavyo haipasi kwa wanaume wawili kumruhusu mwanamke au mbwa au nguruwe kupita mbele yao.” Kila siku asubuhi naomba kwa unyenyekevu: “Hongera kwako Ewe Mungu kuniumba kulingana na matakwa yako” na mwanamme anaomba, “Hongera kwako ewe Mungu kuwa hukuniumba mpagani au mwanamke wala mjinga.”

Joji alikuwa akimuangalia Levi mzuri na macho yake mazuri ya kibuluu yaliyojaa machozi akimsikitikia, kadhalika akausikitikia moyo wake na macho yake na akahisi uhusiano mkubwa wa aliyekuwa akizungumza pamoja na hisia zake Levi za ndani.

Nakuomba msamaha…Je, tunaweza kubadilisha maudhui; kwani nimechoka sana, na nisamehe kwa kukukera.

Nilikuambia hilo toka mwanzo.

Lakini mambo haya yote hayamuhusu mwanamke katika Uyahudi peke yake?

Hapana kabisa… Ni kwenye Uyahudi pekee, ama katika dini zingine ni mambo mengine!! Nataraji hutoghadhibika na kukerwa, mwanamke katika Talmud (nacho ni kitabu cha pili baada ya torati) kinasema: Mwanamke asiyekuwa Mwisrael si chochote isipokuwa ni mnyama tu; hivyo basi kuzini nae sio kuvunja sheria; kwani anatokana na kizazi cha wanyama.

Kasumba ya aina gani hii! Lakini nirudie kusema kuwa sijakinaishwa bado na unayosema, mimi nimesoma kuhusu Uyahudi, na nimesoma sehemu mbali mbali katika torati, lakini pamoja na hayo nahisi unaifasiri torati kama utakavyo.

Sijui kwa nini nimeanza kujielezea na kubwabwaja sana lakini kwa kuliweka wazi: Sisi hatusomi torati kama msomavyo injili.

Kwa vipi?

Torati ni ufunuo kutoka kwa Mungu, wakati ambapo talmud ni sherehe (maelezo) ya torati, wala hatuwezi kuifahamu torati peke yake ukiiweka kando talmud, lakini sipendi kukukera na hilo.

Na ni nani aliyeandika talmud?

Imeandikwa na kalamu nyingi sana zaidi ya miaka elfu moja, kwa nini maswali haya?

Kwa sababu nimekerwa sana, nahurumia hali ya mwanamke, na samahani sijakinaishwa na ulichosema kuhusu mwanamke.

Mengi niliyokuambia nimeyatoa kutoka kwenye torati je unataka kutoka kwenye talmud?! Talmud ina mkusanyiko wa vijitabu sitini na nne (64), je ungependa kusikia chochote kilichomo ndani yake?

Kama halikukeri hilo, tafadhali nijulishe.

Kama ni hivyo sikiliza mambo ya ajabu sasa… katika moja ya vitabu vya Talmud: Ikiwa mbwa atamrukia msichana wakati anapofanya usafi kwenye ardhi na akaingiza utupu wake na kumwingilia basi msichana huyo hazingatiwi kuwa ni mchafu, na anaruhusiwa kuolewa na Rabi (mwanasheria wa sheria za kiyahudi) hata aliyekuwa katika daraja la juu kabisa! Na talmud imeweka umri wa msichana anayefaa kufanya tendo la ndoa akiwa na miaka mitatu tu na siku moja!! Yaani msichana katika umri huu anafaa kuwa mke wa rabi. Ama umri wa mtoto wa kiume ambao unamruhusu kujamiiana inaelezwa na vitabu vya talmud kuwa ni miaka tisa na siku moja, ama baadhi ya rabi wamesema ni miaka minane na siku moja. Katika sehemu nyingine talmud inasema: Mtu anaposimama kujamiiana pamoja na msichana mdogo wa miaka mitatu na siku moja haizingatiwi kuwa ni tendo la jinsia!! Kwa sababu ni kama yule mtu kuweka kidole chake kwenye jicho la msichana!! Ama kijana wa kiume wa umri wa chini ya miaka tisa na siku moja kwa kufanya tendo la ndoa pamoja na mwanamke aliyekwisha baleghe jambo hilo halizingatiwi kuwa ni zinaa!! Kwa sababu ni kama vile amemjeruhi kwa ujiti!! Kama ambavyo talmud haizingatii kuwa tendo la jinsia pamoja na wanyama kuwa ni zinaa wala mtendaji haadhibiwi! Na mwanamke ambae anafanya jinsia na wanyama hazingatiwi kuwa amezini wala haadhibiwi bali anayeadhibiwa ni mnyama! Hali kadhalika haizingatiwi tendo la ndoa na uume uliolala kuwa ni zinaa wala haadhibiwi!

Samahani, hii inatosha; nimeshapatwa na kichefuchefu na mazungumzo haya, lakini nina swali na nisamehe kwa mara nyingine kuzungumza nawe kwa uwazi “Wewe ni mtu mwenye dini au unalipa kisasi juu ya dini ya Uyahudi?!” Narudia kuomba samahani lakini sidhani kuwa Wayahudi wote wako hivi!

Ndio…Mayahudi wote hawako kama nisemavyo, kuna masekula kama sahibu yako Kakhi ambao hawajali torati wala talmud, na kuna makundi mengine mbali mbali, lakini kwa masikitiko nikuwa sisi ni miongoni mwa familia za dini sana na mimi ni mtu wa dini. Hata hivyo sijui kwa nini nimekuambia yote hayo! Huenda nimekuwa nabwabwaja sana kuhusu nafsi yangu na huenda nikawa nimekosea, na huenda nilikuwa nataka kujitetea kwa kuwa kwangu dhaifu kuwa nimekuja kukupa mwili wangu na nilikuwa najihisi kudhalilishwa.

Sijakusudia kukudhalilisha na hii sio tabia yangu, lakini anataka nini kunituma kwako?

Sijui kwa nini haswa, kila ninachokifahamu kutoka kwake ni kuwa una fedha ambayo bado hujampa, na amefahamu kutoka kwako kuwa hutompa hizo fedha hadi nije kukufurahisha kwa kiwiliwili changu.

Kiwiliwili chako ni kizuri sana, kiasi gani natamani kustarehe nacho, lakini… mimi nimeoa na ninachojali ni misimamo yangu, huenda nikawa nashadidia kuliko inavyopasa, na samahani kwani amenifahamu kwa makosa, mimi sikumwambia hivyo, na hainipasi kusema hayo.

Kwa masikitiko mimi ni bidhaa… macho yake yakajaa machozi na hakuweza kumiliki nafsi yake na kuanza kulia: Huenda amekufahamu hivyo kwa sababu ya Kakhi.

Samahani, nyamaza. Nini uhusiano wa kilichotokea na Kakhi?

Kila anapokuja Kakhi anaongea na na mimi nalala kwake siku moja au mbili, Kakhi ni Myahudi; na ana mikataba, mali na wanawake, hivyo basi ni lazima mwakilishi wa Kakhi ahudumiwe kama vile anavyohudumiwa Kakhi, ni udhalili kiasi gani huu!

Joji hakujua aseme nini na haswa alipomuona Levi akilia.. alinyamaza tu huku akiuangalia uzuri wake, kisha akamsikitikia, akahisi dhambi kwani yeye Joji ndie aliyemsukuma katika mazungumzo haya yaliyomjeruhi…..

Futa machozi yako Levi.. Nisamehe sitorudia maneno haya tena unaonaje tukapate kahawa?

Usiombe msamaha… wewe hujakosea.

Walikwenda kwenye mkahawa uliopo hotelini – wakati huo Joji aliazimia kubadilisha maudhui na kuwa mbali na matamanio ya kiwiliwili

Una hofu gani ya kusainiwa mkataba wa ulinzi na shirika letu?

Sina hofu yoyote.

Nimetakiwa nije kutoka Uingereza kwa ajili ya kujibu maswali yako.

Ha ha ha, ukweli ni ili kumletea fedha zake, ikiwa una fedha na ukishampa , basi zingatia kuwa mkataba umeshasainiwa.

Ukweli ninazo, je nikupe wewe au ?

Mpe …kisha akatabasamu kwa huzuni; hata wewe unawatumikia na Kakhi pamoja na kupingana na misimamo yako!

Kwa masikitiko unachosema ni sahihi, kinachotakiwa tuzungumze kuhusu bidhaa yetu na sio kwa rushwa…

Kama ni hivyo Uyahudi sio mbaya kuliko Ukristo!

Huenda, na kwa sababu umekuwa mkweli na mimi kwa kiasi hiki hebu sasa nikueleze ukweli wangu.

Ukweli gani?!

Mimi nipo katika msafara wa kutafuta furaha na hiyo inatokana na hofu na wasiwasi ulionipata baada ya kushindwa kujibu maswali makubwa, nimeanza kufanya utafiti kuhusu dini mbalimbali, utafiti wangu sasa unahusu Uyahudi, kisha utafuatiwa na Ukristo na mwisho kwenye Uislamu.

Furaha ni neno zuri, lakini linaelekea zaidi kuwa la wanaume katika Uyahudi, ni kiasi gani natamani kuwa mwanamme!

Kwani hukufuata dini ili uwe mwenye furaha?

Bila ya shaka, lakini huenda ikawa furaha ya akhera tu.

Sasa kwa nini usibadilishe dini yako?

Uyahudi ni bora kuliko Ukristo na Uislamu, ni dini kongwe zaidi, na watu wake ni wateule, yote niliyokuambia, huenda ikawa ni kubobojoka kwa sababu ya hisia yangu ya kudhalilishwa, samahani. Je huhisi kudhalilika unapotoa rushwa na kwenda kinyume na msimamo wako?!

Ndio, mara nyingi maisha yanatubadilisha kuwa ni vifaa wanavyochezea watu, Ha ha ha, lakini huoni kuwa wachezaji wote huwa ni Mayahudi?!

Ha ha ha, kitu cha kawaida kabisa kwani sisi ni taifa lililochaguliwa…unanitaka niache Uyahudi!

Pamoja na kuwa uzuri wako umejitokeza kwa mara nyingine, na ya kuwa suala la mkataba na maafikiano na maswali mbali mbali tumeyamaliza, Je, utaona kero lau kama tutazungumzia kuhusu Uyahudi zaidi? Tusiingie tena kuhusu maudhui ya mwanamke, mimi nataka kufahamu zaidi juu ya dini yenu kongwe.

Simu ya Joji ililia, aliyepiga simu alikuwa ; Joji akamuomba Levi apokee simu.. alitaka kujua maendeleo ya Joji na Levi, na makutano yao yalikuaje…

Mimi nipo katika hali nzuri na Levi vile vile, na tunaendelea kujadiliana katika kazi zetu.

Ha ha ha, hamjamaliza bado?

Bado…huenda tukamaliza leo.

Mnaweza kumalizia leo au kesho hotelini ukitaka, sisi tupo kuwahudumia.

Vizuri, lakini nataka tukutane kesho ikiwezekana, nina cheki yenu ili tusaini mkataba.

Muda utakaomaliza na Levi mimi nipo kukusubiri.

Asante nitakupigia tupange muda.

Nitasubiri mawasiliano yako, na napendekeza Levi akutembeze katika mji mtakatifu kesho ukipenda.

Sawa, nitapanga nae kuhusu hili.

Sawa, nakuacheni kwa baraka za Mungu.

Joji alimaliza mazungumzo, na akaangalia macho mazuri ya kibuluu ya Levi…

anataka kuwa na uhakika na cheki yake.

Na kuhakikisha kuwa nimetekeleza yote aliyotaka nifanye.

Alitoa pendekezo zuri.

Sidhani kama anaweza kuja na pendekezo zuri, kwani amependekeza nini?

Tutoke kesho ukanitembeze sehemu takatifu.

Vizuri…lakini kitu cha kushangaza, wakati mwingine huja na pendekezo zuri kwa mtu ambae humtarajii hilo.

Sasa hivi ni saa kumi na mbili, ukipenda tumalizie mjadala wetu kuhusu Uyahudi, na kesho nitakusubiri asubuhi kwa ajili ya matembezi ya sehemu takatifu za Kiyahudi.

Vizuri, tumalizie mjadala wetu na napendekeza ziara yetu katika sehemu takatifu iwe kesho kutwa yaani Jumamosi, kisha akacheka kwa kuona haya: Tutakwenda kuangalia sehemu takatifu, na ukitaka kitu kingine ni leo au kesho tu.

Kitu kingine …nimefahamu, wewe ni mzuri sana, lakini nimekuambia kuwa nimeoa na misimamo yangu inanikataza.

Nikuambie ukweli, hao Wakristo waliooa na wenye dini zao hawakatazwi kufanya mambo haya.

Ndio, kwa masikitiko umesema kweli, lakini hilo kwangu halinipendezi, hiyo ni hiana kwa mke wangu, kama nilivyokuwa sipendi afanye yeye hali kadhalika na mimi sipendi kufanya.

Sio nakusifu tu lakini wewe ni mtu mzuri, nimefurahishwa nawe sana.

Waliendelea kuangaliana kwa muda na hakuhisi pindi mikono yake ilipokamata mikono yake milaini, kisha Joji akatanabahi na kuondosha mikono yake na kusema kwa aibu.

Asante sana, wala sidhani kama kuna jambo lenye kuhitaji shukrani, la muhimu mimi naona ni vizuri ziara yetu kama ulivyosema iwe Jumamosi.

Vizuri, tumalize mjadala wetu.

Nataka kufahamu zaidi kuhusu torati na talmud.

Kama nilivyokuambia sisi tunasema kuwa torati imetoka kwa Mungu. Ama talmud ni sherehe (maelezo) au ubainisho na kanuni mbali mbali za torati ambazo zimenakiliwa kwa njia ya mazungumzo na baadae kuandikwa.

Yaani talmud ni maneno ya watu!

Ndio, isipokuwa huwezi kufahamu torati bila kuisoma talmud, sisi sio kama Wakristo kama nilivyokuambia hapo kabla.

Kwa nini msirejee moja kwa moja katika maneno ya Mungu yaliyomo kwenye Torati?

Nimekuahidi kuwa mkweli nawe, hata torati yenyewe ina matatizo mengi, umeona maneno yaliyoandikwa kuhusu mwanamke.

Itakuaje maneno ya Mungu yawe na matatizo? sijafahamu bado!

Kwa masikitiko sisi tunasema kuwa inatoka kwa Mungu lakini kuna dalili zenye kuthibitisha kuwa upotofu umeingia ndani yake.

Dalili za upotofu? Ipo wapi nakala yake ya asili?

Torati ya asili imepotea, lakini kuna nakala tatu tofauti, na baadhi zina jumla zilizozidi zenye kugongana na nakala hizo ni: Nakala ya Kigiriki; nayo ni nakala ambayo imebaki kuwa inazingatiwa kwa Wakristo hadi karne ya kumi na tano na wakati huo huo walikuwa wakiona ile nakala ya Kiebrania kuwa imepotoshwa, hadi hivi sasa Kanisa la Kigiriki linaizingatia kuwa ni nakala sahihi vivyo hivyo makanisa mengine ya mashariki.

Ama nakala ya Kiebrania ambayo inakubaliwa zaidi na Wayahudi na Waprotestant, ina jumla ya safari 39 (vitabu 39), na kulikuwa na makubaliano ya Wakristo juu ya usahihi wa ile nakala ya Kigiriki (Kiyunani) hata katika karne ya kumi na tano, na ya kuwa nakala ya Kiebrania ilipotoshwa na Wayahudi mwaka 130 A.D. kwa makusudi kwa lengo la kuwatia shaka kuhusu ukweli wa nakala ya Kiyunani ambayo Wakristo wakiitegemea wakati ule, kama ilivyoongezwa kuwa upotofu huo ulikuwa unawakusudia Wakristo na Mayahudi wa Samaria kwa pamoja. Hata hivyo baada ya kujitokeza kundi la Protestant katika karne ya kumi na sita mambo yakabadilika; Waprotestant wakaelekea kukubali nakala ya Kiebrania na kusema kuwa nakala ya Kiyunani imepotoka, na mwishowe nakala ya wasamaria; na wasaramia ni kundi la Kiyahudi lililokuwa likiishi katika milima ya Nablus na nakala yao ina vitabu saba tu katika Agano la Kale na kilichozidi baada ya hapo Mayahudi wa Saamira waliona kuwa ni ziada iliyoongezwa (Feki). Na ndani yake kuna jumla mbali mbali na Paragrafu ambazo hazipo katika nakala nyinginezo. Baadhi ya wahakiki wa Kiprotestant wanaizingatia hii zaidi kuliko ile ya Kiebrania pamoja na kuwa katika baadhi ya sehemu wanaitanguliza kuliko ile ya Kiebrania.

Historia ya ajabu sana na migongano yenye kusisimsha lakini ni mambo gani yaliyopotoshwa…tuache maudhui ya mwanamke na mambo ya jinsia.

Mambo mengi!!! Miongoni mwayo ni ile tuliyoitaja asubuhi kuhusu sifa za mungu ambayo hayamfalii, na maovu na machafu na mapungufu ya mitume na….

Samahani kwa kukukata maovu na mapungufu kwa mitume?!

Ha ha ha, unajua!! Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu nazungumza hivi, ukweli mimi nashangazwa na nafsi yangu sana, lakini nahisi kufurahishwa kufanya hivyo je hili linatokana na kushindana au ni wasiwasi wa shetani?! Sijui ila najihisi mwenye furaha kufanya hivyo, niache nikupe mifano: Katika torati Nuhu ameelezwa kuwa anakunywa pombe na kukaa uchi; imekuja ndani yake: “Nuhu alikuwa mkulima akilima mizabibu na kupanda na kunywa pombe na kukaa uchi ndani ya hema lake.”

Ama kuhusu Lut: “Aliishi na binti zake wawili pangoni, binti yake mkubwa akamwambia mdogo: Baba yetu amezeeka na katika ardhi hii hakuna mwanamme wa kutuingilia, tumnyweshe baba yetu pombe, tujamiane nae, wakafanya wakabeba mimba kwa watoto wawili Mawaab na Amuun.” Na mfano wa hayo mengi nadhani mifano hii miwili inatosha.

Samahani Levi, lakini kwa nini unarejea mara kwa mara katika masala haya ya jinsia kila tukiachana nayo?

Kwa sababu nimeiahidi nafsi yangu kuwa mkweli nawe na wewe ndie uliyeniuliza.

Napenda tuingie maudhui mengine.

Levi alitabasamu na mashavu yake yakawa mekundu kwa haya kiasi cha kuonesha uzuri wake zaidi.

Ha ha ha, tafadhali maswali yako yasiwe kuhusu jinsia na mwanamke.

Ombi la Joji halikuwa kwenda mbali na kadhia za jinsia ila kutoroka kuukodolea uzuri wa msichana aliye mbele yake; hakutaka kabisa kusikia hisia za mwili wake na kiu kikubwa kwa uzuri wa kupindukia ulio mbele yake. Hivyo basi aliogopea kumfanyia hiana Katarina na kwenda kinyume na misimamo yake mwenyewe, kisha akakumbuka maneno ya Adam mashuhuri “Furaha katika wepesi (ukawaida)”: akajisemesha mwenyewe: Laiti ningeweza kuishi na misimamo yangu kwa wepesi, akajaribu kubadilisha maudhui.

Uliniambia kuwa wewe ni kutoka Austria.

Ha ha ha, hapana, nimekuambia Israel.

Ndio, nakusudia wazazi wako kutoka Austria, niruhusu nitoe takwimu za Uingereza kulingana na Mayahudi; katika mwaka 1945 Wayahudi walikuwa asilimia 38. Waislamu asilimia 58 na Wakristo asilimia 8. Na kuwa idadi hii kubwa ya Wayahudi ilikuwa ni kwa sababu ya kuhama kiasi cha wayahudi 50,000 hadi 60,000 baina ya miaka 19201945. Sasa mnawaonaje Waislamu na Wakristo kuwa ni magaidi na nyie ndio mliohamia na kukalia kwa mabavu ardhi yao?!

Samahani … nyie Waingereza ndio mnaokalia nchi za watu kwa mabavu, na nyie ndio mliotupa ardhi yetu na kuturudishia haki yetu.

Kwa nini Uingereza imerudisha haki yenu kama msemavyo, je ni huduma ya bure kwenu tu?!

Ninachojali ni ardhi yetu tu na tumerejeshewa, ama kwa nini Uingereza ikatuhudumia hilo ni swali lenu na sio langu…. Pamoja na kuwa Uingereza na Ulaya zimetuhudumia lakini wakati huo huo zimetuuwa sana. Je, hujui hilo?

Unakusudia yale maangamizi makuu yanayofahamika kama Holocaust?!

Sisi ni watu tuliodhulumiwa sana na kuteswa sana katika historia, ama Holocaust ni moja tu ya mtiririko huo wa kuteswa.

Usiku wa jana tu kabla ya kuja huku mke wangu ambae ni Mkatoliki alikuwa ananihadithia mateso ya Wakristo kutoka kwa Mayahudi, kila taifa wanahisi kuteswa.

Swadakta…..hata washenzi Waislamu magaidi waliomuua baba yangu wanasema kuwa wanateswa, lakini historia na hali halisi inakupa ukweli wa mambo.

Wewe umesema unapenda mjadala wala huoni vibaya kuambiwa ukweli, je huoni kuwa Waislamu wameteswa, mmewafukuza na kukalia nchi yao na kuwaua!!

Magaidi wanastahiki hili na zaidi, na nani aliyefanya hivyo! Ni nyie kabla yetu, hivyo msitukosoe.

Umebadilika, sasa unashambulia tu. Ndio, sisi ndio tuliofanya hivi kabla yenu, kwani huoni kuwa wanateswa?

Nimekuambia kuwa wanastahiki hivyo na zaidi ya hayo; wao ni washenzi, wapo nyuma, wanyama magaidi….

Lakini huoni kuwa hata Wakristo Wapalestina nao wanateswa na sio Waislamu peke yao!

Unakusudia Israel na sio Palestina.

Ndio, huoni kuwa Wakristo Israel wanateswa na Mayahudi!

Usighadhibike, Wakristo wanaweza kwenda nchi yoyote Ulaya au Marekani kama hawapendezwi na muamala wetu!!

Ha ha ha, maneno yako makali yenye kukata na yana kinzana kabisa na uzuri wako, sitarajii uzuri wote huu unasema maneno makali kama haya!

Asiyekuwa tayari kutuhudumia juu yetu kumuua!

Haya ndio mafundisho ya kitabu kitakatifu?!!

Ndio, ndani ya torati tunasoma:

Amesema Bwana Mungu wa Israeli; “Kila mmoja na abebe upanga wake na atembee kila sehemu mlango kwa mlango na amuue ndugu yake, rafiki yake na jirani yake.” Vile vile imeandikwa: “nikamsikia anasema: Nendeni mjini nyumba yao wapigeni. Msiwaonee huruma wala kuwasamehe. Waueni Wazee, vijana, wa kike na wa kiume, watoto, wanawake pamoja na wasichana.” Kadhalika imeandikwa: “Sasa nendeni muwapige na waharimishieni kila walichonacho wala usiwasamehe bali muueni mwanamme na mwanamke, mtoto na anayenyonya, ng’ombe, mbuzi, ngamia na punda”. Je inakutosha maandiko haya au niongeze?

Samahani…inaelekea nimekughadhibisha, tulia kidogo bila shaka huu ndio ugaidi wenyewe usiovumilika!

Mimi nimetulia nimekuambia hapo kabla kuwa haya ni maneno ya Mungu yaliyomo ndani ya torati na sio maneno yangu!

Joji alimuita mhudumu, na akataka amletee juisi ya chungwa na kumgeukia Levi ambae alijaribu kuficha wasiwasi wake na hasira zake…

Unataka nini ili utulie zaidi?

Juisi ya ndimu tafadhali.

Joji alinyamaza kwa muda akiwa anamuangalia Levi usoni akiwa anahema kwa nguvu, na kufikiria uzuri aliokuwa nao Levi na upole wake na mazungumzo aliyokuwa akizungumza yasiyokuwa ya huruma…nae Levi alikuwa ni kama mtu aliyepigwa kichwani akawa amejiinamia chini kisha akanyanyua kichwa chake huku akitokwa na machozi….

Baba yangu amekufa, na nimebaki kuwa mwanasesere wa , yote hayo kwa sababu ya mateso ya kihistoria tuyapatayo, kisha unataka niamini kuwa hawa magaidi Waislamu wanateswa!?

Karibu… kunywa juisi ya ndimu na tuachane na maudhui haya madamu yanakukera…

Hayanikeri, na unaweza kukamilisha, na mimi mtulivu mno sasa hivi.

Kwa ukweli, je wewe unakinishwa na maandiko ya torati uliyo yataja?

Ukweli ukweli… hapana.

Kwa nini?

Je, sijakuambia kuwa torati imejaa upotoshaji, ukatili huu hauwezi kutoka kwa Mungu mwenye huruma!

Umesema kweli… Mungu ni mwenye huruma sana kwa waamini wake.

Ili nikurejeshe tena katika jinsia na mwanamke hebu sikiliza yaliyozungumzwa katika andiko hili la torati: “Kuanzia sasa waueni watoto wa kiume na kila mwanamke aliyeingiliwa na mwanamme, ama watoto wa kike na wanawake ambao hawajaingiliwa waacheni kwa ajili yenu.” Kisha Levi akatabasamu kwa mara nyingine na akasema: chukua andiko hili tena: “Wakawausia wana wa wakisema: Nendeni katika mashamba ya mizabibu na jificheni humo, Na subirini hata watakapotoka wasichana wa Shilo kwa ajili ya kucheza nendeni upande wao, watekeni kwa ajili yenu kila mmoja mwanamke mmoja kisha torekeni nao katika ardhi ya i.” Kisha Levi akacheka kwa dharau na kusema: Tumerejea tena kwenye jinsia na wanawake isipokuwa maelezo ya sasa yanahusu kuuwa na kutekwa! Je, tuache tena maudhui haya?

Jambo la kushangaza kabisa! Siamini ninachokisikia! Ndio, tuachane na maudhui haya vile vile, lakini samahani ni nani hawa watoto wa kike wa Shilo? Ni nani hao Shilo?

Shilo ni Wakristo au masaya katika moja ya tafsiri tuliyo nayo, la msingi ni wale wanawake ambao sio Wayahudi kama vile wanawake wenu na wanawake wa Kiislamu, nisamehe kwani umenifedhehesha, na hivyo akili yangu kuchanganyikiwa.

Hamna neno, nadhani wakati umetutupa, nakualika chakula cha usiku ili upate utulivu kisha uondoke…

Ooh …sijatanabahi na muda, sasa hivi ni saa tatu usiku, ikiwa inatoka kwako hamna neno nawafiki, vinginevyo naomba niondoke ukiniruhusu.

Sipendi mazungumzo kwa njia hii, mimi sijaja nikuamrishe nimekuambia kuwa nimefurahi kwa ukweli wako, nimefaidika sana nawe katika njia ya kuelekea furaha, na mimi napenda kukaa nawe ukiwa katika hali ya matakwa yako mwenyewe.

Asante sana kwa wema wako, tutaonana kesho.

Tumekubaliana tuonane kesho kutwa Jumamosi!

Ziara yetu kutembelea sehemu takatifu za Kiyahudi ni kesho kutwa, lakini tunaweza kukamilisha mjadala wetu kesho ukipenda?

Tutakutana kesho nitakapokuja kukutana na asubuhi, lakini ningependa kulitemblea Kanisa la Kiyama na Kanisa la Bikira Maria ikiwezekana.

Kanisa la Kiyama (la siku ya mwisho) sio kanisa la Kiprotestant na wewe unaniambia kuwa ni Mprotestant… kisha akasema: je unanidanganya?

Kwa nini nikudanganye? Nitalitembelea kwa sababu nimemuahidi mke wangu Mkatoliki kuwa nitalitembelea.

Wewe unampenda mke wako sana, nitakutumia dereva saa mbili asubuhi ili akulete ofisini uonane na , na ujitahidi kutoka mapema ili uweze kuyaona makanisa hayo mawili kwani kesho ni Ijumaa.

Ina maana gani kuwa kesho Ijumaa?

Ina maana kuwa ulinzi na vizuizi barabarani ni vingi, ili wahakikishe kuwa magaidi hawawezi kulipua wakati wanapokwenda kuswali swala ya Ijumaa.

Saa mbili nitakuwa tayari ili kuelekea ofisini…kisha akasimama na kumpa mkono Levi akiwa anamuangalia machoni, na kusema: nakushukuru sana na nisamehe kwa kukusumbua.

Mimi haswa ndio wa kukushukuru kwa ukarimu wako na wema wako na ukweli wako na uaminifu wako kwa mkeo na misimamo yako.

Nawe ni mtu mzuri kabisa.

Ni kiasi gani nami natamani kwenda pamoja nawe katika njia ya furaha ambayo unaiendea, ila mazingira yangu hayanisaidii.

Nani anajua? Huenda ukaweza…Tutaonana kesho asubuhi ewe mrembo.

Joji alikula chakula chake cha usiku haraka baada ya kuondoka Levi na sura ya Levi bado ilikuwa machoni mwake, alikuwa akihisi kuwa karibu nae, lakini hakujua ni kwa nini? Je ni kwa sababu ya uzuri wake wenye kufitinisha? Au kuwa kwake mkweli? Au ni kwa sababu tu ya kuvutiwa nae? Alijihisi akiwa ana babaika, anakumbuka tabasamu lake… machozi yake…. Ghadhabu zake na hasira…..yote hayo yalibaki akilini mwake.
Alimsikitikia ya kuwa ni mmoja katika wahanga wa mafundisho yaliyopotoshwa yenye kiza… vipi maskini yule atawezaje kukabiliana na dhulma na mipaka na hata uhuru wake kuchupwa pamoja na haki zake kwa jina la Mungu!!
Alipanda chumbani kwake, na kufungua television akijaribu kumsahau Levi na uzuri wake ili aangalie habari, habari ya magaidi kulipua London ilianza kupungua, lakini aliona na kusikia katika habari hizo kuwa wahusika wa ulipuaji huo walikuwa ni wafuasi wa harakati za SIITA zilizojitenga, na ya kuwa yule Mpakistani aliyekuwa anatafutwa amepatikana; kwani aliogopea tukio lile na kujificha sehemu katika pambizoni mwa London, ambapo baadae aliachiwa huru kwa kuthibitishwa kuwa hakuhusika na chochote… kuhusu Mpakistani yule Joji alijisemea nafsini mwake: Kumethibitika kutohusika kwako ewe Karimullah.
Kisha baada ya hapo ilikuja habari za matayarisho ya serikali ya Israeli kuhusu siku ya kesho Ijumaa. Katika taarifa hiyo serikali iliwakataza watu wote walio chini ya miaka hamsini wasiswali katika msikiti wa Aqswa kwa kuhofia ulipuaji….
Joji alizima televisheni na kufungua barua yake pepe, na kurudisha majibu ya barua alizopokea, kisha aliamua kuandika baadhi ya maandiko ya torati aliyoambiwa na Levi kisha kuzituma kwa Tom pamoja na Adam. Alimaliza kuandika na kuzituma wakati huo ilikuwa ni saa tano usiku, akajiegemeza kitandani alale, lakini ile fikra yake kwa Levi ilikuwa bado haijaondoka, Joji alijiuliza Je, alikosea alipokataa kulala nae! Ingekuwa furaha ya kiasi gani kama angemkubalia, kwani Levi alikwisha kuwa tayari kwa hilo. Hii haikuwa ni mara yake ya kwanza kwani Levi alikwisha wahi kufanya hivyo na mkuu wake wa kazi ambae ni Kakhi, ni maadili gani haya ambayo yanatunyima ladha ya maisha?! Wala Joji hakufahamu kwa nini, muda huo huo akakumbuka wivu wake na hasira zake alipofikiria kuwa Katarina alikuwa akimfanyia hiana pamoja na Tom. Alijisemesha moyoni: Ni mgongano gani ninaoishi? Napenda kufanya hiana lakini wakati huo huo naichukia na ninatoa rushwa na nawaona wanaopokea kuwa hawana maadili, ni kiasi gani natamani kunyooka kwa roho yangu, fikra zangu, maisha yangu na furaha zangu na maadili yangu…

(4)

Ilipofika saa mbili asubuhi Joji alikuwa ameshamaliza staftahi yake, alipanda
chumbani kwake huku akimsubiria dereva afike. Ilipotimia saa mbili kamili simu ilipigwa kutoka mapokezi na kumjulisha kuwa kuna mtu anayemsubiria hapo mapokezi. Alipoteremka kwa mshangao akamuona kuwa aliyekuwa akimsubiria ni Levi na si dereva kama Levi alivyomjulisha jana,

alifurahishwa sana kumuona na kutabasamu kisha kumpa mkono….

Sikutaka kukusumbua

Wewe unastahiki…..Kama ambavyo mjadala wako unanipendeza sana.

Asante sana kwa kunisifu na tabia yako nzuri, je yupo ofisini hivi sasa?

Anakusubiri ofisini, nimemjulisha kuwa utakwenda kwake.

Asante, kwani nimesahau kuwasiliana nae.

Alitabasamu tabasamu zuri lililong’arisha uso wake….

Baada ya kutoka kwako tu na kabla ya kufika nyumbani alinipigia simu ili ahakikishe kama nimelala kwako, hakuamini nilipomwambia kuwa wewe sio Kakhi na wewe hutaki hilo, nikamjulisha kuwa utakuja asubuhi na anaweza kuhakikisha hilo mwenyewe.

Alimuangalia kwa makini huku akisema:

Nani aliyesema kuwa sikutaki?!

Levi alibabaika na usoni mwake ulionekana mgongano wa hisia zake, rai, fikra na matamanio yake…

Unakusudia nini? Je kuna chochote kilichobadilika baada ya kuondoka kwangu?

Ha ha ha, nakutaka wewe na elimu pamoja na utamaduni ulionao na akili na maadili yako. Ama kiwiliwili chako ni johari ambalo natamani kuliangalia kwa umakini na ni kama ua natamani kulinusa, lakini ni fedheha kumuangalia mwanamke kama kiwiliwili tu, na sipendi kukukosa kama nilivyokuwa sipendi kuacha misimamo yangu.

Levi alifuta kwa mkono wake wa kushoto paji lake la uso akiwa ananyanyua fundo la nywele zake.

Ah ah ….sijui kwa nini nimekuwa nina hofu sana?

Je ulimwambia kuwa tumechukua fikra yake ya kwamba tutakwenda kutembelea sehemu takatifu?

Hapana, mjulishe wewe.

Kwa kweli, sijihisi utulivu na , na ninahisi kudhalilishwa kwa kuwa naachana na misimamo yangu na kumpa rushwa, hata hivyo ni kwa sababu sijalifikiria jambo hili kwa utulivu kabla ya kuja kwangu vinginevyo ningekataa, kwa ujumla tumalizie maudhui sasa hivi na baada ya kurejea kwangu tutaendelea kwani kwa kila tukio lina mazungumzo yake.

Vizuri, kwa sababu hujampa fedha ndio maana anadhania sijafanya kazi yangu vizuri.

Maisha ya hovyo ambayo mtu anaachana na misimamo yake kwa ajili ya mali au tamaa ya ngono au kwa sababu ya cheo!

Ninaweza kuonekana kama najigonga mwenyewe, lakini kama sio watu kuachana na misimamo kwa ajili ya mali, matamanio ya kijinsia, basi Israel isingesimama, na kuendelea na kubakia hadi hivi leo.

Ni kiasi gani najihisi kuwa ni mtu wa hovyo nami nikielekea kutoa rushwa, na sijui kwa nini sikufikiria jambo hili aliponiambia Kakhi!

Kwa hali yoyote ile tumeshafika kwenye shirika, utakuta mikataba yote ipo tayari kwa ili usaini.

Natamani tumalize haraka, nahitaji baada ya kumaliza dereva anichukue kutembelea makanisa.

Samahani.. siwezi kukuchukua kukupeleka kwenye makanisa mwenyewe, dereva atakusubiri ili akupeleke.

Joji na Levi waliingia kwa naye alisimama kumkaribisha Joji na kumpa mkono hali ya kuwa ametabasamu…

Siku yenu ya jana ilikwenda vipi? Na usiku wenu ulikuwaje?

Ilikuwa ni siku yenye shughuli nyingi ambapo tumemaliza shughuli yetu na Levi.

Ndio… Levi amenijulisha kuwa upo tayari kusaini mkataba, na ya kuwa umejibu maswali yake yanayohusiana na mambo ya teknolojia, kisha alimgeukia Levi na kusema: Unaweza kumalizia kazi zako hivi sasa kiasi cha mimi na Joji kusaini mkataba.

Nitaondoka; kwani nina kazi…kisha alimgeukia Joji: utakapomaliza kazi zako utamkuta dereva akikusubiri.

Kwa nini dereva? Unaweza kumchukua Levi? Kwani hakukufaa? hakukupendeza?

Tumekubaliana kutekeleza mapendekezo yenu kutembelea sehemu takatifu kesho pamoja, ama leo ningependa kutembelea makanisa matakatifu.

Vipi ilikuaje jana na Levi?

Nzuri sana.

Nilishangaa aliponipigia simu saa tatu unusu usiku na kunijulisha kuwa yupo karibu na nyumbani, ulikuwa unaweza kuchukuwa wakati nae zaidi madamu umenisifia kuwa amekuwa mzuri kwako.

Tulimaliza mjadala wetu saa tatu usiku kisha akaondoka, na nilikujulisha kwenye simu kuwa nataka kukuona ili kusaini mkataba na kumaliza maudhui haya…hii ni cheki nakupa imetoka kwa Kakhi.

Asante sana wewe pamoja na Kakhi, na hii mikataba ipo tayari kusainiwa.

Tumemaliza?

Tumemaliza mikataba, lakini umebakiwa na siku tatu kwetu, mimi pamoja na Levi tupo tayari kukukirimu.

Asante kwa ukarimu wako.

Hata baada ya kumaliza matembezi yenu kesho pamoja na Levi anaweza kuja mkakesha naye hotelini na yeye Levi yupo tayari kwa hilo.

Nadhani nitakuwa mchovu baada ya matembezi, nitahitaji kupumzika na kulala mapema, na sitoweza kukesha!!

Ha ha ha, jaribu akustareheshe Levi… alipokuwa akija Kakhi kusaini mikataba hakuwa akipumzika kabisa ila tu alipokuwa akistareheshwa na Levi.

Tumeshatia saini mkataba na tumemaliza, je ninaweza kuzungumza nawe maudhui mengine yasiyokuwa na mahusiano na mikataba?

Sijafahamu unachokitaka? haya uliza.

Nitasema kwa ukweli kabisa bila ya kukuonea haya: Kwa nini unachukua fedha ili usaini mikataba? je hii sio rushwa?

Ha ha ha, kama unapenda ukweli, kwa nini nawe na Kakhi mnastarehe na Levi ili kusaini mikataba?! je hii nayo sio rushwa ya kijinsia?!

Ndio, ni rushwa ya kijinsia, na hiyo ndio moja ya sababu mimi kukataa kufanya hivyo.

Kakhi hakuwa hivyo, bali akitaka kwa uwazi kabisa, ama kutaka kwako jana ilikuwa ni kwa ishara, pamoja na kama ulivyosema kuwa hukustarehe na Levi na hili ni tatizo lako wewe na kama ni rushwa kama usemavyo kwanini basi umenipa mimi?!

Inaelekea maneno yako ni sahihi na yenye mantiki, kwa nini nitoe kama ni rushwa kwa ujumla je mali na wanawake wanakuletea furaha?

Bila ya shaka, furaha ya duniani ni matamanio ya kijinsia, mali na utawala …kisha akapumua na kusema: hata kama matamanio haya yenyewe yatatuletea tabu na mashaka?!

Sijafahamu itakuwaje ni starehe za maisha na raha zake zikatuletea mashaka na tabu?

Hii ni migongano ya maisha ewe rafiki yangu, mambo ya kijinsia, mali pamoja na utawala ni mambo yenye furaha katika maisha ya kihisia, lakini wakati mwingine yanadhulumu na kuzipa tabu roho zetu, sawa sawa na zilivyo sikukuu zetu zilizokuwa mbali kabisa na furaha. Je sikukuu hazitarajiwi kuwa ni siku zenye furaha zaidi katika masiku yetu? Nitakujibu ndio, lakini sisi kwetu sikukuu zetu ni siku za huzuni kwetu.

Inakuaje hilo?

Levi anaweza kukujibu zaidi yangu … Ha ha ha, nae ni mzuri hali kadhalika, unaweza kukamilisha mjadala nae, katika sehemu ambayo itakupa utulivu.

Nakushukuru sana.

Joji alitoka kwa , na akamuuliza sekretari ilipo ofisi ya Levi, kisha akaenda kwake… aliingia ofisini mwa Levi, akaanza kwa kumuuliza kwa shauku:

Kimetokea nini kati yenu?

Nahisi kudhalilika, nimempa rushwa, na tumesaini mkataba.

Je, umezungumza nae kuhusu rushwa au kuhusiana nami?

Ndio, tumezungumza kuhusu wewe sana, samahani bado ananiaridhia kiwiliwili chako… kisha akatabasamu, na kusema; kipya ni kuwa kanitaka nikuulize baadhi ya maudhui.

Kuniulizia mimi?!

Nilipomzungumzia rushwa alinifedhehesha kuwa mimi na Kakhi tunachukua rushwa, lakini sio rushwa ya mali bali ya kijinsia, kisha akanifedhehesha kwa mara nyingine kuwa mimi ndie ninayetoa rushwa na yeye ndie anayepokea, sote tupo sawa.

Kwa masikitiko ni kuwa mwanadamu wakati mwingine anao uwezo wa kujadili na kuhalalisha makosa yake.

Unamkusudia nani?!

Namkusudia , kisha akanyamaza kidogo na kusema: Na mimi vile vile, na samahani na wewe hali kadhalika.

Joji aliangalia chini ya sakafu kwa masikitiko na kusema:

Umesema kweli .. muda wa kuwa falsafa yetu ya furaha zetu katika maendeleo yetu badili ya falsafa yetu ya kuhalalisha makosa yetu na rushwa?

Lakini hukunijulisha unachotaka kuuliza?

amenijulisha kuwa hii ni tabia ya maisha; nayo ni magumu, furaha na starehe zake ni katika yanayotupa tabu roho zetu, mfano wake ni kama sikukuu zetu zenye kuhuzunisha ambazo zilitakiwa ziwe zenye kufurahisha.

Huenda ikawa katika hali ya upotofu ambayo tumezungumzia hapo kabla, yaani kuwa Uyahudi ni dini ngumu, tatizo sio katika ufahamu wako, bali ni katika ugumu wa ukweli uliopo katika Uyahudi, la msingi ni kuwa sikukuu za kiyahudi ni sikukuu zisizokuwa za furaha bali ni za huzuni mara nyingi.

Kwa nini?

Sikukuu zimewekwa maalumu kwa sababu ya ibada, na ibada ya Mayahudi ni ibada ya kulia na huzuni, je hukuwahi kusikia kuhusu ukuta wa kilio?!. Lakini sikukuu zetu muhimu zaidi ni zile tuziitazo Jumamosi ya Jumamosi yaani siku ya kusamehewa ambapo tunafunga zaidi ya masaa ishirini na nne usiku na mchana wala hatufanyi jambo lolote isipokuwa kuabudu tu. Sikukuu zetu ni nyingi sana, pamoja na haya Mayahudi wengi na haswa zaidi masekula wanazingatia sikukuu hizi kuwa ni siku za likizo na furaha tu, na wao hawafanyi ibada ila mambo ya juu juu tu.

Hili sio muhimu, je inawezekana tuwe na maisha magumu kiasi cha kukosa furaha ila katika yale yanayotupa shida na kutuumiza?!

Kwa masikitiko mara nyingi swali hili ninajiuliza na sikuweza kulijibu pamoja na kuzama kwangu katika torati na talmud. Huenda ikawa hivyo kutokana na ugumu wa nafsi ya kiyahudi au dini ya Kiyahudi, na huenda hili likanihitajia mimi nielimike zaidi ili nifikie katika majibu.

Sijui… lakini nachukia mambo kufanywa magumu, na nadhani halitupeleki popote isipokuwa kwenye tabu tupu.

Nami nachukia mambo kufanywa kuwa magumu, lakini ndio nimeshatumbukia, kwa hali yoyote ile umechelewa kwa Dr. Habib na sasa hivi ni saa nne na muda umeshakutupa mkono, bora umfuate yupo nje anakusubiri.

Ni nani huyo Dr. Habib?

Ni mtafiti wa dini mbali mbali ni Mkristo Mkatoliki… Nimemchagua kwa kuwa naamini ni mtu atakayekufaa kusuhubiana nawe.

Joji alinyamaza kwa muda, hakupenda kumuacha Levi, alijaribu kujaza macho yake uzuri wa Levi, nywele zake zinazoanguka mabegani, macho yake yenye kuthibitisha uhai wake na kiwiliwili chake na mwendo wake unaovutia... Je nilikosea pale nilipokataa kulala nae ili niondoshe kiu nilichokuwa nacho kwenye kiwiliwili changu? Je ni kweli alichokisema kuwa starehe za kiwiliwili zinaipa tabu roho, ooh, nimesahau kujadiliana nae kuhusu jambo hilo!
Levi nae alihisi muangalio wa Joji kwake ni kama vile mtu aliyemkumbatia katika kila sehemu ya kiwiliwili chake, hakujua kwanini alisisimkwa kwa muangalio huu, je Joji anamtaka astarehe nae? Sasa kama ni hivyo kwa nini alimkataa pale mwanzo? Au ni yeye Levi alikataa ili Joji amfuatilie lakini hakufanya hivyo, kisha naye Joji kwanini alimkataa na huku akimuangalia kwa matamanio, je amebadilisha rai yake? Huenda ikawa hivyo, je amfungulie maudhui ili alale kwa Joji leo hii, au afanye nini?!!!

Nakushukuru sana, na nitakusubiri kesho saa mbili asubuhi.

Asante sana Joji.

Joji alitoka na kumsalimia Dr. Habib ambae alimkaribisha, kisha wakaondoka kwenda kwenye gari lake….

Tutaelekea kwanza katika Kanisa la Kiama (ufufuo), kwani leo ni Ijumaa na kuna vizingiti vingi barabarani; na huenda tukachukua masaa mawili.

Masaa mawili?!

Kwa bahati mbaya ndio, kawaida ni mwendo wa dakika arobaini na tano hivi tu, lakini kwa kuwa leo ni Ijumaa njia zote hufungwa kutokana na uchunguzi barabarani.

Pamoja na tatizo la wakati kuwa mkubwa na lenye kuchosha lakini jambo hili linastahiki usumbufu huu. Ugaidi umekuwa ni balaa kwa wanadamu.

Ugaidi wa Waarabu Waislamu.

Ugaidi gani unaouzungumzia?

Samahani, mimi ni Muarabu Mkristo tena Mkatoliki na sio Muislamu, lakini ugaidi wa kweli ni wa dola ya Kiyahudi, kwa nini inawakataza watu kuswali katika misikiti yao, kuna ugaidi gani watu kuswali katika misikiti yao?!

Samahani, mimi sio mtaaalamu wa historia wala siasa wala dini, na inaelekea mbele yangu kuna mtaalamu, lakini hao Waislamu si ndio ambao wanajilipua wenyewe, na wanalipua treni na mabasi kuwaua Mayahudi?!

Swadakta wao wanafanya hivyo, lakini ni kwa nini mtu anafikia kufanya hivyo na kujiua mwenyewe?

Katika uzoefu nilionao ni kuwa mtu hawezi kujiua ila atakapofikia katika hali akaona kuwa mauti ni bora zaidi kwake kuliko uhai.

Sasa ni nini kilichowapelekea Waislamu kufanya hivyo?

Sijui kilicho wapelekea kufanya hivyo?

Ni dhulma, mateso, nchi yao kukaliwa kimabavu na udhalili.

Unaelekea unawatetea sana Waislamu.

Kamwe, mimi sio Muislamu, lakini nawatetea wakazi wote miongoni mwa Waislamu na Wakristo, ambao heshima yao imeondolewa na kuibwa ardhi yao na haki zao, fikiria sisi Wakristo tunafukuzwa na kuhama Palestina na sehemu zetu takatifu zinadhalilishwa.

Lakini nyinyi hamlipui kama Waislamu?

Sisi ni wachache hapa pamoja ya kuwa tunadhalilishwa ila ni afadhali sana kuliko wanavyofanyiwa Waislamu; na yote inatokana na nafasi ya Wakristo ulimwenguni.

Sasa kwa nini wasiwajali Waislamu kama walivyo sehemu nyingine ulimwenguni?!

Kwa uwazi na kwa ufupi: Sisi tunaishi katika ulimwengu ambao hauheshimu isipokuwa nguvu tu.. achana na hilo….je unajua Kanisa la Kiama?

Ndio, kiasi fulani, nimesoma sana habari zake.

Vizuri, pamoja na kuwa wewe ni Mprotestant kama alivyo nijulisha Levi.

Ndio, inaelekea Levi amekujulisha kila kitu.

Namjua Levi tokea miaka mitano iliyopita, na sijamuona alivyomjali mtu kama alivyokujali wewe.

Ama mimi ni jana tu ndio nimefahamiana na Levi, nashukuru kwa wema wake…umefahamiana vipi na Levi?

Alinijia akiwa amechoshwa na dini yake ya Uyahudi na alikuwa anataka kuwa Mkristo, alijadiliana nami sana kuhusu Ukatoliki, Levi ni mpenzi wa mjadala.

Je alibadilika tena kuwa Mkristo?

Bila shaka hapana, hakukinaishwa na Ukatoliki wala Uyahudi pamoja na kuwa yeye ni mtu wa dini sana, na ametoka katika familia ya watu wenye dini, na mtu anayebadilisha dini na kuwa Mkristo anaweza kuuwawa au kufungwa au kuadhibiwa kwa adhabu yoyote ile.

Kwa nini hakukinaishwa na Ukatoliki.

Huenda ni kwa sababu ya migongano iliyopo ndani yake, na huenda ikatokana na tabia ya ugumu wa Uyahudi ulivyo.

Na huenda ikatokana na tabia ya ugumu wa Ukatoliki.

Ha ha ha, huenda ikawa hivyo.

Levi amenijulisha kuwa wewe ni mtafiti wa mambo ya dini mbali mbali.

Ndio, mimi ni mwalimu wa Chuo Kikuu nafundisha somo la historia ya dini mbali mbali.

Je unaweza kunihadithia historia ya dini mbali mbali Palestina?

Maudhui ni mepesi sana, pamoja na ugumu wa kisiasa na wa kidini uliojificha ndani yake.

Napenda wepesi huo … nieleze wepesi wenyewe ulivyo.

Kwa hali ya wepesi kabisa…bila ya shaka ardhi hii ilikuwa imekaliwa kabla ya dini zote, na kila dini ya mbinguni imepita katika ardhi hii takatifu, Uyahudi uliutangulia Ukristo na Uislamu. Kabla ya dini zote hizi kulikuwa kuna watu wanaishi, na kila dini iliyopita ikachukua sehemu ya ardhi hii kwa watu wake kuwa katika dini hiyo, na wote waliweza kuishi pamoja, lakini Uyahudi uliokuja hivi karibuni wakataka wenyewe tu –waishi peke yao na wawaondoshe wengine na wawauwe.

Je Waislamu hawakuwafukuza watu hapo kabla?

Kamwe, Makanisa yetu hayakudhulumiwa tokea wakati alipofika Omar bin alKhatwab.

Vipi kuhusu vita vya msalaba?

Vita kati ya dini mbili na kati ya wakazi wa asili Waislamu pamoja nao baadhi ya Wakristo na kati yao na watu wa msalaba walipokuja kutoka Ulaya, hata hivyo kabla ya hapo watu walikuwa wakiishi pamoja kabla ya kuja watu wa msalaba kutoka Ulaya.

Je Wakristo nao hawakuwatesa Mayahudi.

Pamoja na kuwa mimi ni Mkristo ila ni kuwa katika zama zetu Wayahudi waliteswa Ulaya na sio Palestina, ama nchi hii ni nchi ya kusameheana… Ama hapo zamani dola ya Warumi iliwauwa Wayahudi na kuhalalisha damu zao baada ya Issa kupewa utume na Wayahudi kumkadhibisha.

Inaelekea Uarabu wako unakuvuta uwaonee huruma Waislamu zaidi, kwa sababu Uislamu ni dini ya Waarabu, kuliko hata kwenye Ukristo wako!

Huenda ikawa hivyo, lakini Uislamu sio dini ya Waarabu, Waislamu wengi sio waarabu, nami ni muarabu lakini sio Muislamu, ama kisomi ningependa hata majibu yangu yawe kwa njia ya usomi. Waarabu walifika Yerusalem kabla ya Uislamu, je Ibrahim hakuwa ni baba yake Yaqub na Ismail? nao walikuwepo kabla ya Uislamu na kabla ya Uyahudi?!

Samahani kukukatisha, inaelekea mitaa ya hapa ni ya kizamani sana.

Ndio, tumekaribia mji wa kale ambao una kanisa la Kiama, je hukuona kuwa tumepita zaidi ya vituo kumi na tano vya uchunguzi.

Nasikitishwa na kuhuzunishwa na hali ya watu wazima kuwa katika foleni ya kupekuliwa!

Kilichonisaidia mimi ni Ukristo na nafahamika na askari wa barabarani ndio maana tumepita haraka. Ama watu wazima ni kuwa kuna ambao umri wao chini ya miaka hamsini wanakatazwa kwenda kuswali leo –yaani wanakatazwa kuingia kanisa la kiama hata kama ni mimi na wewe basi tusingeruhusiwa kutokana na taratibu za hapa.

Inaelekea mji huu wa kale una hazina ya kumbukumbu nyingi za Ukristo!

Ndio, hata Waislamu pia.

Na Wayahudi kadhalika.

Wao wanasema hivyo, lakini historia na hali halisi haiwaungi mkono… kisha akatabasamu na kusema: ila ni kuwa nguvu wanayotumia kuungwa mkono ni muhimu zaidi katika ulimwengu huu unaotawaliwa na sheria za msituni.

Unaelekea kuwakosoa sana Wayahudi!

Elimu inasema hivyo, lakini huenda nikawa nawakosoa wao kwa sababu wameichukua ardhi yetu kwa mabavu na wameninyima uhuru wangu wa kuabudu.

Acha hayo kwani kila dini inaona hilo, nadhani tumefika katika kanisa la kiama, au vipi?

Ndio, unaweza kuona kuba yake na misalaba yake kule, tutamalizia sehemu zilizobakia kwa kutembea.

Huogopei Waislamu?

Ukiokoka na Yahudi basi mambo mengine ni mepesi tu, je umewahi kusikia Muislamu amemuua Mkristo Yerusalem?

Walitembea pamoja kidogo, mara mbele yao likajitokeza Kanisa kubwa la kale limejiinamia mbele yao, Joji alishangazwa na mjengo wa Kanisa, na akaendelea kuliangalia kwa mshangao.

Utashangaa zaidi ukiingia ndani.

Tuingie basi.

Walipoingia Joji aliangalia nakshi juu ya ukuta iliyoonesha Yesu akiwa msalabani, na chini yake picha kubwa ya Bikira Maria na picha ya Josefu Seremala.

Naamini kuwa picha hii ingefaa zaidi katika Jumba la Makumbusho! Je picha kama hizi zinafaa kuwekwa makanisani, sehemu maalumu za ibada?

Hii ni tabia yenu nyie Waprotestant hampendi picha makanisani…kisha akatabasamu kwa kebehi na kusema: Mnafanana na Waislamu katika hilo!

Kwa mara ya kwanza mtu ananiambia tunafanana na Waislamu, wakati mara zote tunaambiwa tunafanana na Wayahudi.

Joji aligeuka na kuangalia kwa umakini mkubwa na kwa mshangao –kuba iliyopitisha mwangaza uliokuwa ukienea, na kugawanyika katika mianga kumi na mbili.

Hii ni nzuri sana, ni miongoni mwa maajabu ya ulimwengu, mwanga huu unaoshuka kutoka kwenye kuba inawakilisha jua ambalo linapiga kwenye uwazi uliokuwa katikati ya kuba uliokuwa kileleni, inatokeza na kububujika mianga kumi na mbili, na hii ni dalili iliyo wazi kuwa Yesu amesimama kama alfajiri ya siku mpya, na mitume kumi na mbili: ni kama vile mianga ya imani katika ardhi. Kuba hii ilijengwa na kukamilika tarehe mbili Januari mwaka 1997.

Nzuri sana, unahisi roho ya imani unapofika sehemu hii takatifu.

Pamoja na kuwa nyinyi Waprotestant hampendi sehemu hii sana!

Ha ha ha ni nani ambae hapendi sehemu ambayo ndani yake kuna mbao ambayo Yesu amesulubiwa!

Kanisa hili wanaolijali zaidi ni Wakatoliki na Waorthodoksi.

Waislamu walilivunja hapo kabla! Na wewe unasema kuwa Waislamu hawakuvunja sehemu yoyote ya ibada!

Umesema kweli –lilivunjwa na utawala wa Fatimi…, na katika historia vile vile aliuvunja Uislamu kama alivyo uvunja Ukristo, pamoja na hayo waliruhusu lijengwe baada ya miaka arobaini…Mimi sio Muislamu wala sioni tabu yoyote kuzungumzia dhulma za Waislamu ambazo zilikuwepo katika historia, hata hivyo huwezi hata mara moja kuzilinganisha na dhulma za Mayahudi. Kwa masikitiko nasema kuwa hata kulinganisha na dhulma za Wakristo kwa Mayahudi, kwa mnasaba mtu wa kwanza kujenga kanisa hili ni mtu kutoka Syria na sio Ulaya jina lake lilikuwa ni “Zinobious” mwaka 336 A.D.

Ajabu, hakuna watu wengi kanisani.

Kwa sababu misa inafanywa siku ya Jumapili kama ujuayo, na leo Ijumaa na njia nyingi hazipitiki ila kwa tabu, vinginevyo hili ndilo kanisa linalotembelewa na watu wengi zaidi duniani na sehemu takatifu zaidi Ulimwenguni.

Joji alisali kanisani akitekeleza ahadi ya Katarina, na wakatembea sehemu mbalimbali za kanisa hilo pamoja na Habib ambae alikuwa akijibu maswali yake na kumuelekeza vivutio mbali mbali vya kanisa …kisha wakaondoka ili kwenda katika kanisa la Bikira Maria–Habib alipoangalia saa yake ilionesha kuwa ilikuwa ni saa nane kasorobo….

Nataraji tusije kuchelewa zaidi, tuna muda wa saa hadi saa unusu kufika katika kanisa la Maria, na kurudi tutahitaji saa hadi saa na nusu nyingine, ni matarajio yangu turejee kabla jua halijazama…

Vizuri, samahani ningependa kupumzika garini kidogo kwa muda wa nusu saa hivi, najihisi uchovu.

Vizuri, pumzika.

Joji alijilaza kwenye kiti na kufunga macho yake, alihisi matukio ya safari hii (ya Yerusalem) yakienda mbio mbio, alikumbuka kuwa alimaliza lengo lake la kwanza la safari yake kwa haraka sana, na akakumbuka lengo lake la pili, nalo ni kubaini njia ya furaha, alikumbuka mazungumzo yake na Levi na na Habib vile vile, yote hayo yalikamilika kwa muda wa siku moja na nusu tu. Sasa hajui kutatokea nini baada ya siku mbili na nusu zilizobakia.. alimkumbuka Katarina, Tom na Adam, kiasi gani alitamani kama angekuwa nao wote na wakasikia mazungumzo na mijadala yake, alihisi kupata dozi kubwa kichwani mwake kiasi cha kutoweza kuweka na kuanisha rai yake binafsi katika maarifa na taarifa alizoona na kuzisikia. “Alikumbuka pia maswali yake mbali mbali na akamshukuru Mungu kuwa hayamsumbui tena kama ilivyokuwa hapo kabla pamoja na kuwa hajayasahau…Je hili linatokana kwa sababu anafanya kazi katika njia ya furaha? Lakini maswali yake mbali mbali kuhusu njia ya furaha na maarifa yake mengi bado yanamchosha vile vile, wakati akiwa katika fikra hizi mbali mbali na migongano mara usingizi ukamchukua na akaingia katika ulimwengu wa ndoto.

(5)

Joji alipoamka, aliweka kiti chake vizuri na kumuangalia Habib:

Samahani inaelekea nilikuwa nimechoka!

Inaelekea hivyo.

Oh, nimelala muda wa saa nzima! Muda gani umebakia tufike kanisani?

Imebakia robo saa hivi tu…..kisha akaendelea huku akitabasamu: Inaelekea kuna migongano mingi ya ndani, kuanzia Katarina, Tom, Adam, Kikongwe na Maiko, Jiyostana, Kakhi na Levi…

Umeyatoa wapi majina haya?!

Ulikuwa unayataja mara kwa mara ulipokuwa umelala.

Inaelekea nimechoka kweli, nahisi matukio na maarifa mbali mbali kuingiliana kichwani, kadhalika nahisi mwili wangu mzito sana.

Ikiwa mtu hajaweza kutatua kadhia zake za ndani na fikra zake basi zitaingia kwenye nafsi yake na roho yake na kumsumbua.

Hili huenda likawa ndio tatizo langu haswa.

Kwa mnasaba nimefurahishwa na neno ulilotumia mara kwa mara.

Lipi hilo?

Njia ya furaha, ulikuwa unasema mara kwa mara nataka njia ya furaha, neno zuri sana.

Unaonaje tuzungumzie kuhusu njia ya furaha, nataka kukuuliza swali?

Karibu uliza.

Je wewe ni mwenye furaha?

Swali kubwa sana, je linawezekana kujibika?

Ndio, nadhani linawezekana.

Dini zote, fikra nyingi na madhehebu tofauti zinataka hilo.

Wewe ni mwalimu wa historia ya dini mbali mbali ni dini ipi ipo karibu zaidi na furaha?

Kwa mara ya kwanza naulizwa swali hili kubwa…kwa muda mrefu nimejitahidi kufikia jibu hilo, na bado naendelea kufanya utafiti huo.

Je unadhania mtu anaweza kufikia njia hiyo bila haja ya kuwa na dini?

Hili haliwezekani kabisa, elimu itathibitisha kuwa watu wengi katika hao wakanao dini ni wagonjwa wa maradhi ya nafsi na maradhi ya kiakili na ya kuwa wao ni waongo kwa ukanaji wao wa dini.

Sijafahamu …waongo katika ukanaji wao wa dini?!

Yaani wanajifanya kukana dini, na ndani ya nafsi zao wanamuamini Mwenyezi Mungu Muumba, mtoa riziki, ukweli wa ukanaji dini ni kuikimbia dini na majukumu yake… si dini wala itikadi.

Ikiwa dini ndio njia ya furaha, kwa nini basi hawezi kunijibu swali hilo mtafiti na msomi wa dini mbali mbali.

Ni haki yako kusema haya, nami naendelea na utafiti wangu, na hivi karibuni nitafikia kwenye jibu.

Niahidi kuwa utaniambia utakapofikia kwenye jibu hilo.

Ninakuahidi, inaelekea unafuatilia mambo ya dini mbali mbali kama alivyonielezea Levi.

Sipendi migongano, wala sipendi kuyafanya mambo kuwa magumu, napenda akili, roho na kiwiliwili ziwafikiane, kadhalika pamoja na misimamo na raha zake, na napenda ukawaida pamoja na umakini.

Vizuri, napenda unachokipenda, unaelekea ni mwana falsafa, ni lazima tumalize mjadala wetu lakini inaelekea kuwa tumefika katika kanisa la Maria Magdalena, hili hapa mbele yako.

Ni uzuri ulioje mjengo wake!

Hii ni fani ya ujenzi kutoka Russia, amejenga Alexandria, Mrusi na Kuba yake ya dhahabu yenye kupendeza juu ya jabali la mzaituni.

Kama ni hivyo ni Kanisa la karibuni sana?

Ukililinganisha na kanisa la kiama, ndio bila shaka, Kanisa la kiama limejengwa mwaka 335 A.D na kanisa la Bikira Maria limejengwa mwaka 1886 A.D. na baina ya kanisa hizi mbili ni miaka 1500.

Nashangazwa kuwa alama za dini yetu ya Ukristo zimewekwa miaka mingi baada ya kufa kwa wenyewe kitu ambacho mtu anaweza kushuku utukufu wake!

Kwa masikitiko maneno yako ni sahihi kwa asilimia mia moja, bali hata kitabu kitakatifu ni hivyo hivyo. Tafadhali karibu ndani kwani tumefika na hayo mengine tutamalizia tutakaporudi, natamani tumalize upesi kwa ajili ya kurudi kabla ya jua kuzama.

Vizuri, tumalize haraka iwezekanavyo.

Walitembelea kanisa haraka haraka, na kitu kilicho mvutia Joji zaidi ni kuwepo kwa picha nyingi katika sakafu la kanisa, na Joji jambo hilo halikubali kama linafaa katika nyumba za ibada…kama vile alivyovutiwa na mapambo mazuri na kuba zake saba zilizokuwa zinamulikwa na jua, lilikuwa ni jengo zuri, Joji aliswali haraka haraka kisha wakatoka.

Jengo zuri sana.

Ndio; ni katika majengo mazuri sana.

Ama nyie Wakatoliki mnapenda sana picha katika sehemu za ibada, ama mimi sioni kama hii inafaa katika sehemu ya ibada na yananikumbusha mahekalu ya wapagani.

Kwanza:Kanisa hili si la Kikatoliki bali la Kiorthodoksi. Pili: Nimekuambia kuwa katika hili mnafanana na Waislamu.

Siyo Kanisa la Kikatoliki?! Kwa nini basi Katarina mke wangu ametaka nisali humo?

Sijui.

Kwa kuwa wewe ni mtafiti na mwanazuoni wa dini mbali mbali; je unaweza kunielezea tofauti iliyopo kati ya Orthodoksi, Ukatoliki na Uprotestant kwa mtazamo wako?

Swali gumu na jibu tata.

Kwani hupendi mambo mepesi? Ni wepesishie mimi.

Nitajaribu, lakini kwa ujumla kuna tofauti mbali mbali na makundi mengi sana, nitafupisha kwa muhtasari katika makundi matatu makubwa uliyoyataja:

Kwanza: Orthodoksi, yaani ni rai iliyokuwa sahihi au ya haki au iliyojulikana au iliyokamatana na asili ya dini na zote zinafanana nazo ni asili ya mwanzo, na ndani yake limetoka Ukatoliki; na maana yake ni, ‘ya jumla’ au ya ulimwengu tokea mwaka 451 A.D. na kutoka katika Ukatoliki likagawika Uprotestant baada ya harakati za islahi za kidini zilizoongozwa na Martin Luther ambazo zilisambaa Ulaya ya Magharibi kati ya karne mbili; karne ya kumi na nne na kumi na saba.

Hivyo basi asili ni Orthodoksi na sio nyinyi Wakatoliki?

Ndio, pamoja na kuwa tukiwalinganisha nanyi, sisi ndio wa asili na wa mwanzo zaidi kwenu Waprotestant, Ha ha ha, la muhimu Orthodoksi huitwa kanisa lao kuwa ni Kanisa la Mashariki au Kanisa la Kiyunani au Kanisa la Roma la watu wa Mashariki na wafuasi wao ni watu wa Roma ya mashariki; yaani mashariki ya Ulaya kama vile Warusi, nchi za Balkani na Ugiriki, makao makuu ya kanisa ni mji wa Constatinople, na wenye kufuata madhehebu haya ni kanisa la Misri, Armania na wa Ethiopia, ama idadi yao inafikia watu bilioni moja.

Inaingia akilini watu milioni elfu moja!

Ukatoliki, na kanisa lao linaitwa kanisa la Magharibi, na nchi hizo za Magharibi ni kuanzia Latin katika nchi za Italia, Ubelgiji, Ufaransa, Hispania, Ureno, Brazil. Kadhalika wana wafuasi–Ulaya na Amerika ya Kaskazini na Kusini, Afrika na Asia na wanadai kuwa mwanzilishi wake ni Mtume Peter mkubwa wa wafuasi wa Yesu, na ya kuwa Mapapa wa Roma ni wafuasi wao; na wanadai wao kuwa mama wa Makanisa na walimu wao. Kanisa hili linafuata utaratibu wa Kipapa na linaongozwa na Papa, na mkusanyiko wa Makanisa una haki ya kutoa matakwa ya Kipapa nayo kwa muono wao ni matakwa ya Kiungu; kwa sababu Papa ni mfuasi wa Peter mwanafunzi wa MasiyaYesu na wasii wake, na kwa ajili hiyo yeye ni mwakilishi na Mungu, huyo basi matakwa yake hayana mjadala na wafuasi wa madhehebu haya wanafikia milioni elfu moja (Bilioni moja).

Vizuri, kamilisha kuhusu Uprotestant.

Uprotestant; huitwa Kanisa la Kiinjili kwa maana ya kuwa wafuasi wa kanisa hili wanafuata injili na wanaifahamu wao wenyewe bila hata ya kuwafuata watu wengine au kundi jingine, wala hawaamini kuwepo kwa ufunuo wala maono kwa watu wa kanisa, kwa ujumla wao ni wakristo, kwani wanaamini itikadi za msingi, na hawaamini kuwepo kwa siri nyingi za kanisa na ibada mbali mbali na sala zilizoratibiwa kanisani na mambo ya kuiga tu kwa mkumbo ….na walikataa baadhi ya vitabu katika kitabu kitakatifu na itikadi mbali mbali zilizoonekana kuwa ni takatifu.

Mnataka kututoa kwenye Ukristo, hamna neno, ni nini tofauti za kimsingi kati ya makundi hayo matatu?

Nimetaja tofauti za kimsingi na uliposema: Mnataka kututoa katika Ukristo, ukweli ni kuwa tofauti ni nyingi mno baina ya makundi haya kiasi cha kuwa wengine wameona kuwa ni dini tofauti na sio dini moja yenye makundi mbali mbali.

Vipi? Nibainishie?

Kila itikadi ya Kikristo ina tofauti na makundi mengine, na haiwezekani kuzichambua na sisi tukiwa garini, wao wanatofautiana kuhusu Mungu kuhusu Yesu na kuhusu kitabu kitakatifu na kuhusu ibada mbali mbali na mengineyo mengi sana.

Itakuaje dini ikawa ni moja na tofauti zikawa nyingi kiasi hiki? Hapana shaka kuwa mojawapo ni sahihi.

Fikra ya kuwa mojawapo ndio sahihi ndio kisa cha vita na ugomvi kutoka katika makundi haya.

Vita?!

Ndio, vita vilivyoua mamilioni ya watu, kwa mfano vita vya miaka thelathini kati ya mwaka 1618 hadi 16 48 vilivyopiganwa kati ya Protestant na Katoliki na nchi zingine washirika zilizoungana nazo, na vita hivyo viliondosha roho nyingi za Wazungu wa Ulaya yapata mamiloni ya watu, bali nchi ya Ujerumani peke yake walikufa nusu ya watu wake na wakazi wake kupungua kutoka watu milioni ishirini hadi kufikia milioni kumi na tatu na nusu!

Mazungumzo yale yalimchoma sana Joji; kwani anachukia ugaidi wa sura zote. alijiuliza: Je, njia ya furaha inaweza kuwa imejaa damu? Rehema zako Mungu wangu, wanadamu hawawezi kuwa na furaha katika unyama wa aina hii…

Unyama gani huo?!

Historia imethibitisha kuwa tofauti za kidini na itikadi mara nyingi zinabadilika kuwa ni migongano katika uhalisia, tukipenda jambo hilo au tukikataa.

Historia ya ugaidi inasumbua sana!

Ndio kwa masikitiko, na mara nyingi migongano ya kidini huwa ni mikali zaidi na yenye kuchosha kuanzia vita vya Mayahudi vya kuwatesa Wakristo na kumuua Yesu, kisha Wakristo nao kuwatesa Mayahudi, kisha Mayahudi tena kuwatesa Wakristo na Waislamu.

Kwa mara nyingine tena hukutaja mateso waliyoteswa Wakristo na Wayahudi na Waislamu.

Kwa sababu jambo hilo silijui katika historia, je unaweza kunipa mifano?

Waislamu kuvunja Kanisa la Kiama.

Kuna matukio mengi kama haya, mimi nazungumzia mateso ya jumla na mauaji na kuwakataza watu wasifanye ibada, Uislamu umekataza kuvunja nyumba za ibada na makanisa ya Wakristo na kuwaua, kilichotokea katika hayo huwezi kuita ni mateso.

Inaelekea wewe ni Muislamu uliyejificha katika Ukristo.

Ha ha ha, huenda ikawa hivyo, nani anajua, huenda nikawa Muislamu au Protestant siku moja. Je sikukuambia kuwa nyie mnafanana na Waislamu hampendi masanamu wala picha katika sehemu za ibada, kisha akamgeukia Joji na kusema:Au huenda nikawa pamoja nawe katika njia ya furaha, umenikumbusha… ni kipi kisa cha njia ya furaha?!

Njia ya furaha kisa chake ni kirefu mno.

Nifupishie na unielezee.

Kwa ukweli nimechoshwa sana na maswali yenye utata kuhusu maisha, maswali yenyewe ni: Kwa nini tumeumbwa? Nani katuumba? Kwa nini tunaishi? Mwisho wetu ni nini? Na nikafahamu kuwa sitoishi maisha ya furaha hadi nijibu maswali haya yenye utata; hivyo basi nikaanza kutafuta njia ya furaha, kisha akatabasamu na kusema: Na yale majina uliyoyasikia kutoka kwangu usingizini yalikuwa ni majina ya watu niliokutana nao katika njia hii ya furaha.

Na je ziara yako ya mji mtakatifu na mijadala yako ni sehemu ya utafiti wako wa njia ya furaha?

Nimekuja kikazi, lakini kilichonisukuma zaidi ni hicho ulichokisema.

Lini utaimaliza njia hii?

Sijui, lakini nasisitiza kufikia, kisha akatabasamu na kumgeukia, na kusema: Na njia ya furaha yenyewe ni njia nzuri!

Inaelekea mimi, wewe na Levi kuna kufanana sana.

Ki vipi?

Alinijia mimi akitafuta furaha lakini si katika Uyahudi, hata hivyo Ukatoliki haukumkinaisha na mimi nilikuwa Muorthodoksi na kubadilika kuwa Mkatoliki na bado naendelea na utafiti.

Ujaribu Uprotestant – huenda ikawa ni kimbilio lako, mara nyingi namwambia mke wangu Mkatoliki kuwa dini yenu ni ngumu kwa ibada nyingi na siri nyingi zisizo za kimantiki.

Huenda ikawa hivyo, umefikia wapi katika njia ya furaha?

Samahani, je, tumekaribia hotelini? Nadhani naumwa, mwili wangu wote ni mzito sana na nahisi kizunguzungu kwa mbali.

Hamna neno, mungu akubariki, imebakia robo saa hivi.

Nakushukuru sana nimefaidika sana nawe.

Bali wa kushukuriwa ni Levi aliyenitambulisha nawe, nawe itabidi umshukuru, kwani amekujali sana.

Ndio, Levi ni msichana mzuri na katika wasichana wachache wa aina hii, nami namshukuru sana.

Kama vile unampenda, kwani hukuniambia kuwa umeoa?

Ndio, mimi nimeoa, ni msichana mzuri sana, lakini pamoja na uzuri wake wa kupindukia naipenda roho yake zaidi kuliko ninavyokipenda kiwiliwili chake.

Inaelekea wewe una mapenzi ya KiPlato (yaani mapenzi ya taamuli)!

Ha ha ha, au ni mtu mgumu au mgonjwa kama wanavyonisema wanaonifahamu.

Katika jamii yetu ya kimada, kiwiliwili hutangulizwa kuliko roho, katika ibada na katika starehe vile vile, hii ni kwa wengi wetu na huenda ikawa kwa Wayahudi ni zaidi.

Kwa vipi?

Muono wa Kikristo huangalia mambo kwa njia ya kiroho zaidi, lakini jamii yetu ya kimada hujali zaidi furaha za kiwiliwili juu ya hesabu ya furaha za kiroho, historia ya Uyahudi inathibitisha kuwa wao wana muono wa kimada katika kila kitu; Kuhusu mungu, siku ya mwisho, tabia na maadili ya watu, kila kitu kinaweza kuuzwa na kununuliwa, na sikusudii kuuza na kununua mali tu.

Je sijakuambia kuwa unaukosoa sana Uyahudi?.

Unaweza kujadiliana na Levi kuhusu hilo; yeye ni msichana mzuri wa Kiyahudi na yeye hawezi kuukosoa Uyahudi, na unaweza kuiangalia historia na hali halisi ilivyo.

Umenipa hoja kama ilivyo ada yako, je tumefika kwani nimechoka sana?

Dakika chache tu tutafika.

Simu ya Joji iliita alikuwa ni Levi kwa sauti yake nzuri.

Hallo Joji.

Hallo Levi.

Safari yenu imekuaje?

Nzuri sana, kwa nini isiwe hivyo nami nipo katika usuhuba mzuri wa Dr. Habib!

Natarajia kuwa uchaguzi wangu ulikuwa mzuri.

Nzuri kabisa, asante sana.

Nilitaka kutumaini hali yako kabla jua halijazama na kuingia Jumamosi.

Nashukuru hali yangu ni nzuri, asante kwa mawasiliano, na nakushukuru kwa mipango yako mizuri, kesho tutaonana saa ngapi?

Muda wowote utakaotaka, natamani sana tuonane.

Nami hali kadhalika, ahadi yetu kesho saa tatu, nimechoka kidogo na ninataka kupumzika zaidi.

Joji alihisi kubabaika na akamuangalia Habib akamuona ametabasamu.

Pole, Mungu akuhifadhi, je nikuitie daktari?

Asante Levi nakushukuru sana, utanikuta katika afya njema na mchangamfu nikiwa tayari saa tatu.

Kwa heri.

Asante, kwa heri.

….Mazungumzo mazuri kabisa yenye hisia za ndani!!

Unakusudia nini ?

Hamna kitu, Levi ni msichana mzuri sana kama usemavyo.

Unakusudia nini?

Nilikuwa nakutania tu, inaelekea Levi amevutiwa nawe sana, kama wewe ulivyovutiwa nawe, na kila mmoja katika ninyi anajitahidi kumpendezesha mwingine kwa roho yake na kwa fikra zake na maadili yake …kisha akatabasamu na kusema:Na kila mmoja amevutiwa na kiwiliwili cha mwenzake vile vile, hivyo chunga mipaka isije ikawa mapenzi ya roho yakahamia katika mapenzi ya kiwiliwili, au kuthubutu kufanya jambo msilolitaka na kuondokana na kujivua na misingi yenu ya kimaadili ambayo Levi amenihadithia, kwa ujumla tumefika hotelini.

Asante kwa nasaha zako za kweli lakini ambazo ni ngumu, karibu tafadhali tule chakula pamoja, sote hatujala hadi sasa.

Wewe umechoka, nami hali kadhalika, nataraji utanisamehe kwa hili.

Asante, nimefaidika nawe sana, hii hapa ni kadi yangu, kuna mawasiliano yangu, natumaini mawasiliano baina yetu yataendelea…..Ha ha ha, kesho nitakuwa na Levi siku nzima na si vibaya ukawa mlinzi wetu.

Najua kujali kwako tamaduni, fikra, na maadili, lakini nakutahadharisha kama nilivyomtahadharisha Levi kuchanganya mambo wakati mwingine, hali kadhalika sisi ni wanadamu na tuna udhaifu wetu wa kibinadamu, asante sana natamani kuonana kabla ya kusafiri kwako… hii ni kadi yangu..tafadhali nijulishe kila mara umefikia wapi katika njia yako ya furaha.

Joji alipanda chumbani akiwa amechoka sana –alikoga kwanza –kisha kama ilivyo ada yake alifungua Televisheni na kuangalia taarifa ya habari ambayo haikuwa na habari mpya, kisha akafungua kompyuta yake ili afuatilie barua zake pepe, alipata barua kutoka kwa Adam ikisema;

“Baada ya maamkizi: Nimeangalia nukuu za torati zilizochafuliwa ulizonitumia na nikaona hazivumiliki wala haziaminiki, asante kwa kunitumia na tutazungumzia baada ya kurejea kwako, nataraji utaendelea kunitumia barua kama hizi; Mimi nimefaidika nazo sana.”

Kisha aliona barua kutoka kwa Tom inayosema:

“Baada ya maamkizi: Ama nukuu mbali mbali za torati; nilikuambia hapo kabla kuwa dini zote hazifai hazina manufaa yoyote, na ulikaribia kubadilisha rai yangu kabla ya kuja barua hii, nadhani umeanza kukinaishwa na maneno yangu, na usisahau kuwa Wakristo wanaamini Agano la Kale ambayo ndio torati unayoikosoa, ahadi yetu ni Jumanne saa nane mchana ili tujadiliane hilo, kama una mambo mengine nitumie.”

Joji alitaka kumtumia uzoefu alioupata leo hii, lakini hakuweza; uchovu ulimzidi sana na akaamua kuwatumia wote pamoja barua fupiBaada ya salamu aliandika:

“Nimesoma majibu yako na nitajaribu kuwatumia habari moja baada ya nyingine, leo nilishughulishwa sana kama jana, na ilikuwa ni kuhusu itikadi za dini mbali mbali, na migongano ya dini mbalimbali na mateso ya dini moja kwenda kwa wafuasi wa dini zingine. Kadhalika na tofauti kati ya makundi mbali mbali ya Kikristo na mengineyo, na kwa sababu ninajihisi uchovu sana, nitajaribu kesho kukutumia nilichofikia.”

Alifunga kompyuta yake na kujitupa kitandani, hata hivyo alishangazwa kuwa pamoja na uchovu wote alionao lakini Levi na tabasamu lake angavu pamoja na macho yake ya kibuluu havikumuacha akilini mwake. Alikumbuka maneno ya Habib kuwa wakati mwingine mambo huchanganyika lakini pamoja na hofu yake alijiamini na kumuamini Levi vile vile.