Tabia za Utume.

Tabia za Utume.
“Kwa hakika mimi nampenda Muhammad: Sababu ni ile tabia yake safi aliyonayo na mawazo na fikra zake. Kwa hakika mtoto huyu wa majangwani alikuwa ni mwanamme mwenye rai huru: Hujitegemea mwenyewe tu wala hajidai yasiyokuwepo, hakuwa mwenye kiburi!! Hata hivyo hakuwa dhalili, akisimama na nguo zake zenye viraka kama vile alivyompatia Mola wake na kama alivyotaka mwenyewe. Huzungumza na wafalme wa Kirumi na wa Kiajemi kwa maneno yake yenye kutetemesha anawaelekeza maisha haya na maisha ya akhera. Alikuwa anajua uwezo wa Nafsi yake, alikuwa ni mtu mwenye kupitisha azma yake, hacheleweshi kazi ya leo hadi kesho.”


Tags: