kuhitajia binandamu Dini

kuhitajia binandamu Dini

kuhitajia binandamu Dini

Je, mwanadamu ana haja ya dini?

$Einstein.jpg*

Einstein

Mwanazuoni wa Fizikia
Matokeo Imara
“Imani ni matokeo imara na matukufu zaidi katika tafiti za kisayansi.”

Mwanadamu kwa hali yoyote hawezi kuishi bila Dini, na kwa sababu mwanadamu ni mtu mwenye tabia ya kuingiliana na watu na hawezi kuishi peke yake huku akijitenga na jamii, nae vile vile katika maumbile yake ni mtu mwenye dini hawezi kuishi maisha ya sawa sawa bila kuwa na dini, swala la mtu kuwa na dini ni suala la kimaumbile na tabia ya asili ya mwanadamu na hakuna dalili kubwa yenye kuthibitisha hilo kuliko ile hali ya mwanadamu kumtegemea Mwenyezi Mungu katika hali ya shida na dharura, Allah Ta’ala amesema, “Na wanapo panda katika marikebu, humwomba Mwenyezi Mungu kwa kumsafia ut’iifu. Lakini anapo wavua wakafika nchi kavu, mara wanamshirikisha.” (29:65)

Kama ambavyo mtu aliyetengeneza mashine ndiye mwenye kufahamu zaidi mahitajio yake vivyo hivyo na muumbaji huwajua zaidi viumbe wake na mahitaji yao, “Asijue aliye umba, naye ndiye Mjua siri, Mwenye khabari? ”(67:14)

Na kwa sababu Muumba ni Mrehemu na Ghafuri Mkarimu; amewawekea watu sharia ya Dini ili Nafsi zao zihuishwe na maisha yao yadhibitiwe, Allah Ta’ala amesema, “Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele….” (8:24),

Na kwa hilo basi hata yule ambaye anakwenda kinyume na maumbile sahihi na anadai kumkana Allah Ta’ala, wao ni ndani ya Nafsi zao wanajua uongo wa kukana kwao, Allah amesema, “Na wakazikataa kwa dhulma na kujivuna, na hali ya kuwa nafsi zao zina yakini nazo. Basi angalia ulikuwaje mwisho wa mafisadi!” (27:14)

$Dale_Carnegie.jpg*

Dale Carnegie

Mwandishi wa Kimarekani.
Mtu wa Dini na Mgonjwa
“Nakumbuka yale masiku ambayo hakukuwepo na mazungumzo ya watu isipokuwa kuhusu ugomvi baina ya elimu na dini. Mgogoro huu uliisha bila kurejewa, kwani elimu ya sasa ya tiba ya nafsi inatoa habari nzuri kuhusu misingi ya dini. Kwanini?!! Kwa sababu matabibu wa nafsi wamegundua kuwa kuwa imani yenye nguvu na kushikamana na dini na swala hutosheleza kushinda wasiwasi, khofu na msongo wa mawazo na kutibu nusu ya maradhi ambayo tunayoyalalamikia. Hadi Dr. A. A. Bell akasema: ”Kuwa mtu mwenye kushikamana na dini hasumbuliwi na maradhi ya nafsi.”

Na huenda hilo likaonekana kwa uwazi zaidi wakati wa zahama na matatizo zaidi, Allah amesema, “Sema: Mwaonaje ikikujieni adhabu ya Mwenyezi Mungu, au ikakufikieni hiyo Saa - mtamwomba asiye kuwa Mwenyezi Mungu, ikiwa nyinyi ni wakweli? Bali Yeye ndiye mtakaye mwomba, naye atakuondoleeni mnacho mwombea akipenda. Na mtasahau hao mnao wafanya washirika wake.” (6:41-42)

Kadhalika katika Surat Zumar amesema: “Na taabu inapo mfikia mtu humwomba Mola wake Mlezi naye ameelekea kwake. Kisha akimpa neema kutoka kwake, husahau yale aliyo kuwa akimwitia zamani, na akamfanyia Mwenyezi Mungu washirika ili apoteze watu njia yake. Sema: Starehe na ukafiri wako kwa muda mchache. Kwani hakika wewe utakuwa miongoni mwa watu wa Motoni. ” (39:8).

Wanadamu wote wapo katika maumbile ya asili waliyoumbwa nayo na Allah Ta’ala katika kumuabudu yeye kwa mkono wake kheri na shari kufanya ayatakayo na kuhukumu atakavyo, Allah Ta’ala amesema: “Na ikiwa Mwenyezi Mungu akikugusisha madhara, basi hapana wa kukuondolea hayo ila Yeye. Na ikiwa akikugusisha kheri, basi Yeye ndiye Mwenye uweza wa kila kitu.” (6:17)

$Dale_Carnegie.jpg*

Dale Carnegie

Mwandishi wa Kimarekani
Kuwa Mbobezi
“Mwanafalsafa Francis Becon alisema kweli aliposema, “Falsafa ndogo humpelekea mtu kwenye kumkana Mungu. Ama kubobea katika falsafa humrejesha mtu kwenye dini.”

Na katika Surat Faatwir amesema: “Rehema ambayo Mwenyezi Mungu anawafungulia watu hapana wa kuizuia. Na anayo izuia hapana wa kuipeleka isipo kuwa Yeye. Naye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hikima.” (35:2).

Mtu atawezaje kuifikia furaha kwa uwezo wa elimu na matakwa yake??

Mwanadamu ana nguvu za aina mbili: Nguvu ya elimu na nguvu ya matakwa yake, na kwa kadiri ya juhudi yake katika kutekeleza nguvu hizo mbili mwanadamu huyo hufikia malango yake aliyojipangia na vivyo hivyo ndivyo mwanadamu apatavyo furaha.

Ama nguvu ya kwanza (nguvu ya elimu) kwa kadiri ya maarifa yake kwa Allah, kwa majina yake na sifa zake, na yanayopasa kwake katika maamrisho na makatazo, kitabia na kimaadili na vipi ilivyo njia ya ukuruba na kuwa juu ya daraja za mwenye kufuata, na yote yenye kupelekea katika elimu ya ndani kuhusu Nafsi za wanadamu na maradhi yake na jinsi ya kuyashinda hayo, na kwa maadui zake na kila chenye kuzuia baina yake na Mola wake, mbali na mtu kukwea daraja za juu za kutakasa tabia yake iwe ya kiungu kiasi cha kupanda juu kufikia roho za juu na hima za juu, mbali kabisa na mambo ya hovyo kwa lengo la kupata maslahi ya kidunia na matamanio yake, kwa kiasi hicho ndio kimada unapokuwa daraja ya uja wa mtu kwa Allah Ta’ala na nafasi yake, bali na furaha yake duniani sembuse ya akhera.

Nguvu hii ya kielimu ndio masurufu na msaada wa nguvu ya matakwa ya mtu, ambayo yatamuongoza katika uongofu pamoja na kuthibiti na kufanya mambo mazuri, Allah Ta’ala amesema: “Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele….”” (8:24)

$Dr._Douglas_R._ Archer.jpg*

Dr. Douglas R. Archer

Meya wa Regina
Ukweli Ulio wazi Zaidi
“Utafiti wangu kwa ajili ya kupata shahada ya uzamifu (PhD) ilikuwa kuhusu Malezi na kujenga Ummah. Nimegundua kuwa nguzo za Kiislamu za msingi zimeweka misingi mikuu na kanuni madhubuti ili kurudisha jengo la Ummah kijamii, kiuchumi na kiroho.

Na haya madhehebu ya wakanayo Mungu na Dini yanatangaza kufilisika kwao kwa kutekeleza kwao raha za kiwiliwili sembuse kushibisha mahitajio ya kiroho, madhehebu haya yameshindwa kabisa kumhakishia mwanadamu furaha ya kweli vyovyote watakavyopeana kauli nzuri na kupamba kauli zao kwa ghururi.

Mwanadamu anamuelekea nani katika matatizo yake na misiba yake! Anategemea nguzo imara, anaelekea kwa Allah Ta’ala; penye nguvu, matarajio, subira na kutegemea kwema na kumwachia mambo yote yeye. Allah amesema; “Wale walio amini na zikatua nyoyo zao kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu. Hakika kwa kumkumbuka Mwenyezi Mungu ndio nyoyo hutua! ” (13:28).

$Dale_Carnegie.jpg*

Dale Carnegie

Mwandishi wa Kimarekani.
Kushika Dini ni tiba ya Maradhi
“Matabibu wa nafsi wamegundua kuwa imani madhubuti na kushikamana na dini inamtosha kushinda khofu, wasiwasi na msongo wa nafsi na kuponya maradhi haya.”

Hadi hapo atakapoonja uchungu wa moto kwa dhulma ndipo atakapokuwa na yakini kuwa ulimwengu huu una Mola, na ambaye anamnusuru aliyedhulumiwa hata kama, ni baada ya muda kupita, na ya kuwa kuna siku ya mwisho ambayo kila mmoja atalipwa alichokichuma, na mtu mwema kulipwa mema yake na muovu kulipwa maovu yake na hivyo basi kifua chake kuwa imara kwa tumaini na yakini kwa Allah. Allah Ta’ala amesema: “Je! Aliye yafuata ya kumridhisha Mwenyezi Mungi ni kama yule aliye stahiki ghadhabu ya Mwenyezi Mungu, na makaazi yake yakawa Jahannamu? Napo ni mahala pabaya pa kurejea. ” (3:162).

Inakuwaje mwanadamu kama atapoteza dini?

$William_James.jpg*

William James

Mwanazuoni wa Elimu nafsi (Saikolojia) wa Marekani.
Tibu mwenyewe nafsi yako.
“Kwa hakika tiba kubwa zaidi ya nafsi ni kumuamini Mwenyezi Mungu.”

Kinyume na yaliyotangulia; yule ambaye amepoteza maarifa yake kwa Allah Ta’ala na kumuamini basi mtu huyo amepoteza nguvu zake zote, na kadhalika atakuwa amepoteza raha, tumaini na furaha, na atakuwa anaishi baina ya hamu na huzuni, hana utulivu ndani ya nafsi yake, hamu yake kubwa ni kutekeleza na kufanikisha matamanio yake hajui malengo ya maisha yake, wala maana ya kuwepo kwake hapa ulimwenguni. Bali mtu huyu anaishi akibabaika hajui afanye nini, akitafuta furaha, akifuata matamanio yake, lakini anarudi nyuma kiasi cha kuwa ni mnyama au aliyepotea zaidi, Allah Ta’ala amesema: “Au wewe unadhani kwamba wengi wao wanasikia au wanaelewa? Hao hawakuwa ila ni kama nyama hoa tu, bali wao wamepotea zaidi njia.”(25:44),

$Alija__Ali_Izetbegovic.jpg*

Alija ‘Ali Izetbegovic

Rais wa zamani wa Jamhuri ya Bosnia Herzegovina.
Havipo pamoja
“Madhehebu ya Kiyakinifu (unaotanguliza anasa za dunia) siku zote wanathibitisha ambacho wanashirikiana baina ya mwanadamu na mnyama. Wakati ambapo dini inasisitiza kinachotenganisha baina yao.”

Na ikitokea mtu huyu kapatwa na msiba basi kuangukia kuwa ni muhanga wa angamizo la nafsi na angaiko na babaiko lake la ndani, “Na atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu.”. (20:124)

$Henry_Ford.jpg*

Henry Ford

Mwanzilisi wa Shirika la Ford la Magari Marekani
Matabibu wenye kutoa mawaidha
“Kwa hakika matabibu wa nafsi ni watu wenye kutoa mawaidha kwa njia mpya; Kwani wao hawatuhimizi dini kwa sababu ya adhabu ya motoni huko akhera, bali wao hutuusia kushikamana na dini ili tusipate adhabu ile ile ya moto hapa duniani, kama vile moto wa vidonda vya tumbo na msongo wa nafsi na wendawazimu.”

Ni tofauti kubwa sana baina ya mtu mwenye kumjua Mola wake, na kujua ukubwa wake na akajua kinachompasa kwake kwa Mola wake na kuijali kwake kumridhisha Mola wake, akifuata sheria zake, akitii maamrisho yake na kuacha makatazo yake, Na akajua kuwa ni mwenye haja ya kudumu kwa Mola wake katika madogo na makubwa, katika mambo dhalili na matukufu, na katika kila wakati Allah Ta’ala amesema: “Enyi watu! Nyinyi ndio wenye haja kwa Mwenyezi Mungu, na Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kujitosha, Msifiwa.”(35:15).

$Arnold_Toynbee.jpg*

Arnold J. Toynbee

Mwanahistoria wa Uingereza.
Dini ni Maisha
“Dini ni katika vipaji muhimu vya mwanadamu. Tunatosheka kusema kuwa mtu kukosa dini humsukuma kwenye hali ya kukata tamaa kiroho, inamlazimisha kutafuta nguvu ya kidini kwenye sahani zisizomiliki chochote ndani yake.”
$Dr._ Rene_ Dubos.jpg*

Dr. Rene Dubos

Mwanasayansi aliyepata tuzo ya Nobel
Zama za Babaiko
“Kwa hakika sisi tunaishi katika zama za babaiko, wala hapana shaka kuwa mafanikio ya Sayansi na teknolojia zimemzidishia mwanadamu anasa na starehe lakini kwa upande mwingine haikumuongezea furaha na utulivu bali kinyume chake imemuongezea khofu, babaiko, kukata tamaa na maradhi ya nafsi yamemuondoshea maana nzuri ya maisha haya.”

Na mtu mwingine dhana na mawazo yamemtupa katika taabu na kiza na shida, akipapasa kwa kupepesuka kama vile kipofu hapa na pale, moyo wake ukiwa umejaa shaka na wasiwasi, kila akijaribu kukamata au kushika furaha anajikuta yupo katika mazigazi baada ya mazigazi, na hata akipata ladha za dunia na matamanio yake, na hata akipanda cheo na daraja za juu, Je, mtu atakayemkosa Allah atapata nini? Na atakayempata Allah atakuwa amekosa nini?